• Wasiliana na sisi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Handeni Town Council
Handeni Town Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Mji Handeni

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Fedha na Biashara
      • Mipango,Takwimu na Ufuatiliaji
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo,Umwagiliaji na Ushirika
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Elimu Msingi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Maji
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Ardhi na Maliasili
      • Elimu Sekondari
      • Usafi na Mazingira
    • Vitengo
      • Teknolojia,Habari na Mawasiliano
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • Ugavi
      • Nyuki
      • Sheria
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya kitalii
    • kilimo
    • ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • fedha na uongozi
      • mipango miji na mazingira
      • uchumi afya na elimu
      • ukimwi
      • maadili
    • Ratiba
      • vikao vya waheshimiwa madiwani
      • kuonana na mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma Kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Miongozo Mbalimbali
    • fomu mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za Shughuli za Ofisi au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha
    • Matukio

Kamati ya Fedha na Utawala yaridhishwa na utekelezaji wa Miradi ya Maendeleo

Posted on: November 19th, 2018

Kamati ya Fedha na Utawala  katika Halmashauri ya Mji Handeni  imeridhishwa na kupongeza hatua ya utekelezaji wa miradi mbalimbali ya maendeleo.

Hayo yamejiri leo wakati ikifanya ziara ya kutembelea na kukagua miradi mbalimbali ya maendeleo iliyotekelezwa katika kipindi cha robo ya kwanza ya mwaka wa fedha 2018/2019.

Wajumbe wa Kamati hiyo wakiongozwa na Mwenyekiti wa Halmashauri Mhe.Twaha Mgaya ambaye pia ni Diwani wa Kata ya Kwenjugo walijionea hatua za ujenzi wa vyumba viwili  vya madarasa katika Shule ya Msingi Lumbizi iliyopo Kata ya Kideleko ambapo kwa kiasi kikubwa vimekamilika, mradi ambao bali ya kutekelezwa na Serikali pia nguvu za Wananchi zimechangiwa.

Kukamilika kwa miundombinu hiyo ya kutasaidia kupunguza msongamano wa wanafunzi kutokana na uhaba wa vyumba vya madarasa na hivyo kutekeleza kwa ufanisi sera ya elimu bila malipo.

Vyumba viwili vya madarasa katika Shule ya Msingi Lumbizi mara baada ya kutembelewa na Kamati ya Fedha na Utawala.

Pia kamati hiyo ilitembelea miradi ya vikundi vya wanawake na Vijana katika Kata za Kwenjugo, Mdoe na Chanika ambapo Halmashauri kupitia Idara ya Maendeleo ya Jamii kwa kutumia mapato yake ya ndani inatoa mikopo ya riba nafuu kwa vikundi hivyo.

Katika Kata ya Kwenjugo Kamati ilitembelea kikundi cha Mshikamano kinachojishughulisha na shughuli utengenezaji wa bidhaa mbalimbali za mikono kama vile mikoba mikubwa na midogo ya akina mama, sabuni, kapeti ndogo za mlangoni na bidhaa nyingine kutokana na mahitaji ya mteja.Wakizungumza wakati wa ziara hiyo Wanakikundi hicho wamesema bado wanaendelea kutafuta soko la bidhaa zao nje na ndani ya Handeni ambapo kwa kuanzia tayari wamepata soko Mkoani Arusha ambapo wamepewa tenda ya kutengeneza kapeti ndogo za mlangoni mia mbili.

Baadhi ya bidhaa mbalimbali hapo juu zinazotengenezwa na kikundi cha Mshikamano kilichopo Kata ya Kwenjugo.

Katika kufuatilia kama fedha zinazotolewa na Serikali kwa walengwa Kaya maskini kwa ufadhili wa Mfuko wa Maendeleo ya Jamii (TASAF), Kamati ilimtembelea mnufaika Mwanaidi mkazi wa Mtaa wa Kwedigongo katika Kata ya Kwenjugo.

Mlengwa huyo katika kumfuatilia ameonesha mafanikio kwa kuboresha makazi yake ambapo amejenga nyumba ya bati vilevile kupitia TASAF katika maeneo yao Mwanaidi amesema wameamua kuanzisha  vikundi vya ujasiliamali ambapo kwa kuanzia wameanza na ufugaji wa mbuzi.

Bi Mwanaidi mlengwa wa Kaya maskini akieleza jambo mbele ya Kamati ya Fedha na Utawala wakati za ziara

Aidha, miradi mingine iliyotembelewa ni pamoja na ule wa Ujenzi wa vyumba vya madarasa katika Shule ya Msingi tarajali Kwelale, Ujenzi wa Jengo la Ofisi ya Halmashauri, kikundi cha vijana kinachojishughulisha na utengenezaji wa fenicha mbalimbali za majumbani kilichopo Kata ya Chanika pamoja na kikundi cha kina mama seuta kinachoshughulika na ufugaji wa Samaki pamoja na vitalu vya miti

Matangazo

  • KUITWA KWENYE USAILI 2 October 03, 2024
  • KUITWA KWENYE USAILI 1 September 27, 2024
  • TANGAZO LA MAJINA NA MIPAKA YA MITAA September 16, 2024
  • Angalia zaidi

Habari Mpya

  • HOSPITALI YA HALMASHAURI YA MJI HANDENI IMETOA ELIMU YA KUJINGA KWA MAGONJWA YA KUAMBUKIZA KWA WAFANYAKAZI WA BOMBA LA MAFUTA WILAYA YA HANDENI EACOP

    March 21, 2025
  • BARAZA MAALUMU LA MADIWANI LAPENDEKEZA KUONGEZEWA MAENEO YA UTAWALA

    March 14, 2025
  • MKUTANO MKUU WA 39 WA JUMUIYA YA TAWALA ZA MITAA TANZANIA (ALAT)

    March 11, 2025
  • ZIARA YA MHE. RAIS DKT SAMIA SULUHU HASSAN

    February 25, 2025
  • Angalia zaidi

Video

Mbunge wa jimbo la Handeni Mjini Mh.Reuben Kwagilwa aliamsha Bungeni
More Videos

Viunganishi vya Haraka

  • Dira na Dhamira
  • Kupata leseni ya Biashara
  • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
  • Kumuona Mkurugenzi
  • Kupata kibali cha Matangazo
  • Muundo wa Tasisi
  • Kumuona Mwenyekiti wa Halmashauri

Viunganishi Linganifu

  • Sekretariti ya Ajira
  • Ofisi ya Rais - Ikulu
  • FFARS-LIVE
  • PLANREP- BAJETI 2020/21
  • TAMISEMI
  • Utumishi

Watembeleaji wa Dunia

world map hits counter

Idadi ya waliotembelea tovuti

free HitCounter

Ramani

Wasiliana na sisi

    Barabara ya Korogwe - Handeni

    Anuani ya Posta: S.L.P 51 HANDENI

    Simu ya Mezani: 027-2641807

    Simu ya Mkononi:

    Barua pepe: td@handenitc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera za faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Copyright ©2022 GWF . All rights reserved.