Halmashauri ya Mji Handeni ipo kati ya nyuzi za Latitudo 4° 55’ na 6° 04’ Kusini na kati ya nyuzi za Longitudo 37° 47’ na 38° 46’ Mashariki mwa Meridiani Kuu ya Greenwich.
Makao Makuu ya Halmashauri ya Mji Handeni yapo katika Kata ya Kwenjugo Mtaa wa Ngugwini. Halmashauri ya Mji Handeni haina pwani na ipo katika kimo cha kati ya mita 600 hadi mita 1,000 kutoka usawa wa bahari.
Takribani asilimia 70 ya wakazi wa Halmashauri ya Mji Handeni wanajihusisha na shughuli za kilimo na ufugaji, asilimia 27 wanajishughulisha na biashara ndogo ndogo na ajira binafsi (maduka, wafanyabiashara, vibarua) na asilimia 3 wameajiriwa katika sekta za umma.
Halmashauri ina ukubwa wa Hekta 64,750 ambapo eneo linalofaa kwa kilimo na mazao mchanganyiko ni hekta 48,577.5. Mchanganuo wa maeneo mengine ni kama ifuatavyo;
Barabara ya Korogwe - Handeni
Anuani ya Posta: S.L.P 51 HANDENI
Simu ya Mezani: 027-2641807
Simu ya Mkononi:
Barua pepe: td@handenitc.go.tz
Copyright ©2022 GWF . All rights reserved.