• Wasiliana na sisi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Handeni Town Council
Handeni Town Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Mji Handeni

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Fedha na Biashara
      • Mipango,Takwimu na Ufuatiliaji
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo,Umwagiliaji na Ushirika
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Elimu Msingi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Maji
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Ardhi na Maliasili
      • Elimu Sekondari
      • Usafi na Mazingira
    • Vitengo
      • Teknolojia,Habari na Mawasiliano
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • Ugavi
      • Nyuki
      • Sheria
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya kitalii
    • kilimo
    • ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • fedha na uongozi
      • mipango miji na mazingira
      • uchumi afya na elimu
      • ukimwi
      • maadili
    • Ratiba
      • vikao vya waheshimiwa madiwani
      • kuonana na mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma Kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Miongozo Mbalimbali
    • fomu mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za Shughuli za Ofisi au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha
    • Matukio

Halmashauri ya Mji Handeni yapongezwa kwa kupata hati safi

Posted on: May 23rd, 2018

Baraza la Madiwani katika Halmashauri ya Mji Handeni limekutana kwa ajili ya kuwasilisha na kupokea taarifa za utekelezaji wa miradi ya maendeleo ya Kata zake mbalimbali.

Katika kikao hicho cha kujadili taarifa za robo ya tatu Januari hadi Machi kwa mwaka wa fedha 2017/2018, Mwenyekiti wa Halmashauri ,Twaha Mgaya ameipongeza Halmashauri ya Mji Handeni kwa kupata hati safi kutokana na ripoti ya Mdhibiti na mkaguzi mkuu wa hesabu za Serikali (CAG), Twaha ambaye ni Diwani wa Kata ya Kwenjugo aliwaomba madiwani waendelee kushikamana na kushirikiana na Wataalam wa Halmashauri ili waendelee kuwahudumia Wananchi katika Kata zao ili kuleta maendeleo katika Halmashauri ya Mji Handeni.

Kwa upande wake Mkurugenzi wa Halmashauri Bw.Kenneth Haule amewaomba madiwani katika Kata zao washiriki kikamilifu kwenye miradi ya maendeleo inayotekelezwa katika maeneo hayo ili utekelezaji wake uwe wa kiwango kinachokubarika ikiwa ni pamoja na kukamilika kwa wakati ."Waheshimiwa katika maeneo yenu kuna miradi mbalimbali ya maendeleo  inatekelezwa lakini katika taarifa zilizowasilishwa hapa kutoka kwenye Kata zenu zijaona suala la miradi ya maendeleo likiripotiwa kwa kina ,mfano hatua ilipofikia,mipango endelevu kukamilisha baada ya Serikali kuchangia kiasi kikubwa cha fedha ",amesema

Mwenyekiti wa Halmashauri mhe.Twaha Mgaya akisoma sala ya kuiombea Halmashauri kabla ya kufungua Baraza

Wahe.Madiwani wakiuatilia mkutano wa Baraza 

Wageni pamoja na wahe.Madiwani wakifuatilia mkutano wa Baraza wakati ukiendelea

Baadhi ya wageni waalikwa wakifuatilia mkutano wa Baraza ukiendelea

Vilevile  Baraza limepongeza wanafunzi wenye mahitaji maalum wanaosoma katika Shule ya Msingi Chanika walioshiriki mashindano ya michezo ya watu wenye mahitaji maalum ngazi ya Wilaya,Mkoa mpaka kitaifa kwa kufanikiwa kuiletea heshima Halmashauri ya Mji Handeni kwa kufanikiwa kunyakua medali kwenye michezo mbalimbali walioshiriki ikiwemo mpira wa miguu,pamoja na kukimbia, miongoni mwa medali zilizonyakuliwa na vijana hao ni pamoja na medali ya dhahabu.

Akizungumza kwenye Baraza hilo Mwl.Mkuu Shule ya Msingi Chanika wanaposoma vijana hao amesema" wanafunzi wenye mahitaji maalum kumbe na wao mwenyezi mungu amewajaalia vipaji mbalimbali ikiwemo michezo hivyo basi wakipewa nafasi wanafanya makubwa kama walivyofanya hawa ni vizuri kuendelea kuwawekea mazingira rafiki kulingana na mahitaji yao,naishukuru Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania inayoongozwa Dkt John Magufuli kwa kuendelea kutuletea fedha za chakula kwa wanafunzi hawa".

Kwa upande wa Halmashauri wametoa zawadi mbalimbali kwa wanafunzi hao pamoja na walimu wao ikiwemo fedha tasilimu kwa kila mtu.

Mwl.Shule ya msingi Chanika akipokea zawdi kutoka kwa Mwenyekiti wa Halmashauri

Mwl.na kocha wa wanafunzi wenye mahitaji maalum akipokea zawadi kutoka kwa Mwenyekiti wa Halmashauri



Pichani hapo juu baadhi wanafunzi wenye mahitaji maalum walioshiriki michezo wakipokea zawadi zao 

Matangazo

  • KUITWA KWENYE USAILI 2 October 03, 2024
  • KUITWA KWENYE USAILI 1 September 27, 2024
  • TANGAZO LA MAJINA NA MIPAKA YA MITAA September 16, 2024
  • Angalia zaidi

Habari Mpya

  • HOSPITALI YA HALMASHAURI YA MJI HANDENI IMETOA ELIMU YA KUJINGA KWA MAGONJWA YA KUAMBUKIZA KWA WAFANYAKAZI WA BOMBA LA MAFUTA WILAYA YA HANDENI EACOP

    March 21, 2025
  • BARAZA MAALUMU LA MADIWANI LAPENDEKEZA KUONGEZEWA MAENEO YA UTAWALA

    March 14, 2025
  • MKUTANO MKUU WA 39 WA JUMUIYA YA TAWALA ZA MITAA TANZANIA (ALAT)

    March 11, 2025
  • ZIARA YA MHE. RAIS DKT SAMIA SULUHU HASSAN

    February 25, 2025
  • Angalia zaidi

Video

Mbunge wa jimbo la Handeni Mjini Mh.Reuben Kwagilwa aliamsha Bungeni
More Videos

Viunganishi vya Haraka

  • Dira na Dhamira
  • Kupata leseni ya Biashara
  • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
  • Kumuona Mkurugenzi
  • Kupata kibali cha Matangazo
  • Muundo wa Tasisi
  • Kumuona Mwenyekiti wa Halmashauri

Viunganishi Linganifu

  • Sekretariti ya Ajira
  • Ofisi ya Rais - Ikulu
  • FFARS-LIVE
  • PLANREP- BAJETI 2020/21
  • TAMISEMI
  • Utumishi

Watembeleaji wa Dunia

world map hits counter

Idadi ya waliotembelea tovuti

free HitCounter

Ramani

Wasiliana na sisi

    Barabara ya Korogwe - Handeni

    Anuani ya Posta: S.L.P 51 HANDENI

    Simu ya Mezani: 027-2641807

    Simu ya Mkononi:

    Barua pepe: td@handenitc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera za faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Copyright ©2022 GWF . All rights reserved.