• Wasiliana na sisi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Handeni Town Council
Handeni Town Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Mji Handeni

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Fedha na Biashara
      • Mipango,Takwimu na Ufuatiliaji
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo,Umwagiliaji na Ushirika
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Elimu Msingi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Maji
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Ardhi na Maliasili
      • Elimu Sekondari
      • Usafi na Mazingira
    • Vitengo
      • Teknolojia,Habari na Mawasiliano
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • Ugavi
      • Nyuki
      • Sheria
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya kitalii
    • kilimo
    • ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • fedha na uongozi
      • mipango miji na mazingira
      • uchumi afya na elimu
      • ukimwi
      • maadili
    • Ratiba
      • vikao vya waheshimiwa madiwani
      • kuonana na mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma Kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Miongozo Mbalimbali
    • fomu mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za Shughuli za Ofisi au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha
    • Matukio

HALMASHAURI YA MJI HANDENI KUSHIRIKIANA NA WADAU KUDHIBITI UGONJWA WA KIFUA KIKUU

Posted on: January 24th, 2025

Hospitali ya  Halmashauri ya Mji Handeni imezindua rasmi Kampeni ya “Catch-Up” yenye lengo la kuimarisha juhudi za kutambua na kudhibiti ugonjwa wa kifua kikuu. Kampeni hii inalenga kugundua wagonjwa wapya 99 wa kifua kikuu ndani ya mwaka, kwa kuhakikisha uchunguzi wa mapema na matibabu sahihi kwa wagonjwa wanaogundulika, ili kupunguza maambukizi mapya.

Akizungumza wakati wa uzinduzi wa kampeni hii, Bwana Jonas Mkondya kwa niaba ya Mganga Mkuu wa Hospitali ya Halmashauri ya Mji Handeni alisisitiza  umuhimu wa juhudi za pamoja katika kupambana na ugonjwa wa kifua kikuu, ambao takwimu zinaonyesha kuwa mgonjwa mmoja wa kifua kikuu cha mapafu ambaye hajagunduliwa anaweza kuambukiza watu takriban 10 ndani ya mwaka mmoja.

Kampeni hii inalenga makundi yaliyo hatarini zaidi, ikiwemo watoto wanaoishi na wagonjwa wa kifua kikuu, watu wanaoishi na virusi vya UKIMWI (VVU), wafungwa, na watu wanaoishi katika maeneo yenye msongamano kama machimboni na masokoni. Katika Halmashauri ya Mji Handeni, maeneo yaliyoathirika zaidi ni Kideleko, Kwedigongo, Kwaluwala, Msaje, Zizini, na Bwila.

Huduma za uchunguzi wa kifua kikuu zinapatikana katika Hospitali ya Mji Handeni, Kituo cha Afya Kideleko, na Zahanati ya Msekwa, ambapo teknolojia kama GeneXpert, TruNat, mionzi ya X-ray, na dadubini hutumika. Hata hivyo, sampuli kutoka maeneo mengine bado husafirishwa hadi vituo hivi kwa ajili ya uchunguzi.

Takwimu za UgonjwaKwa wastani, Halmashauri ya Mji Handeni hugundua wagonjwa 130 wa kifua kikuu kila mwaka. Kwa sasa, kuna wagonjwa 74 walioko kwenye matibabu, mmoja kati yao akiwa ni mgonjwa wa kifua kikuu sugu.Halmashauri imeweka mikakati mbalimbali ya kudhibiti ugonjwa huu, ikiwemo chanjo ya BCG kwa watoto wachanga, tiba kinga kwa watoto chini ya miaka 5 na wagonjwa wa VVU, pamoja na utoaji wa elimu kuhusu kifua kikuu katika vituo vya afya na mashuleni.

Kwa kushirikiana na wahudumu wa afya ngazi ya jamii, kampeni hii itahakikisha inafikia maeneo mbalimbali, ikiwa ni pamoja na masoko, machimboni, shule za bweni, minadani, na kupitia ufuatiliaji wa nyumba kwa nyumba.Uzinduzi huu umeonyesha dhamira ya dhati ya Halmashauri ya Mji Handeni ya kuimarisha afya ya jamii kwa kudhibiti ugonjwa wa kifua kikuu kupitia ushirikiano wa karibu na wadau mbalimbali. Kampeni hii ni hatua muhimu katika kupunguza ugonjwa wa kifua kikuu katika Handeni Mjini.

Matangazo

  • KUITWA KWENYE USAILI 2 October 03, 2024
  • KUITWA KWENYE USAILI 1 September 27, 2024
  • TANGAZO LA MAJINA NA MIPAKA YA MITAA September 16, 2024
  • Angalia zaidi

Habari Mpya

  • HOSPITALI YA HALMASHAURI YA MJI HANDENI IMETOA ELIMU YA KUJINGA KWA MAGONJWA YA KUAMBUKIZA KWA WAFANYAKAZI WA BOMBA LA MAFUTA WILAYA YA HANDENI EACOP

    March 21, 2025
  • BARAZA MAALUMU LA MADIWANI LAPENDEKEZA KUONGEZEWA MAENEO YA UTAWALA

    March 14, 2025
  • MKUTANO MKUU WA 39 WA JUMUIYA YA TAWALA ZA MITAA TANZANIA (ALAT)

    March 11, 2025
  • ZIARA YA MHE. RAIS DKT SAMIA SULUHU HASSAN

    February 25, 2025
  • Angalia zaidi

Video

Mbunge wa jimbo la Handeni Mjini Mh.Reuben Kwagilwa aliamsha Bungeni
More Videos

Viunganishi vya Haraka

  • Dira na Dhamira
  • Kupata leseni ya Biashara
  • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
  • Kumuona Mkurugenzi
  • Kupata kibali cha Matangazo
  • Muundo wa Tasisi
  • Kumuona Mwenyekiti wa Halmashauri

Viunganishi Linganifu

  • Sekretariti ya Ajira
  • Ofisi ya Rais - Ikulu
  • FFARS-LIVE
  • PLANREP- BAJETI 2020/21
  • TAMISEMI
  • Utumishi

Watembeleaji wa Dunia

world map hits counter

Idadi ya waliotembelea tovuti

free HitCounter

Ramani

Wasiliana na sisi

    Barabara ya Korogwe - Handeni

    Anuani ya Posta: S.L.P 51 HANDENI

    Simu ya Mezani: 027-2641807

    Simu ya Mkononi:

    Barua pepe: td@handenitc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera za faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Copyright ©2022 GWF . All rights reserved.