• Wasiliana na sisi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Handeni Town Council
Handeni Town Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Mji Handeni

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Fedha na Biashara
      • Mipango,Takwimu na Ufuatiliaji
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo,Umwagiliaji na Ushirika
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Elimu Msingi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Maji
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Ardhi na Maliasili
      • Elimu Sekondari
      • Usafi na Mazingira
    • Vitengo
      • Teknolojia,Habari na Mawasiliano
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • Ugavi
      • Nyuki
      • Sheria
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya kitalii
    • kilimo
    • ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • fedha na uongozi
      • mipango miji na mazingira
      • uchumi afya na elimu
      • ukimwi
      • maadili
    • Ratiba
      • vikao vya waheshimiwa madiwani
      • kuonana na mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma Kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Miongozo Mbalimbali
    • fomu mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za Shughuli za Ofisi au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha
    • Matukio

Kamati ya fedha na utawala yatembelea miradi mbalimbali ya Maendeleo inayotekelezwa

Posted on: November 11th, 2017

Kamati ya fedha na utawala kwa kuambatana na wataalam mbalimbali kutoka Halmashauri ya Mji Handeni wamefanya ziara ya ukaguzi wa miradi ya maendeleo kwa lengo la kujua hali halisi ya miradi,Mahali ilipofika na thamani ya pesa iliyotumika (value for money).

Maeneo yaliyotembelewa na Kamati ya fedha na utawala ni pamoja na eneo la ujenzi wa Ofisi mpya za Halmashauri ya Mji Handeni,Ujenzi wa matundu ya vyoo katika Shule za Msingi Antakae,Misima na Kwakivesa,Ujenzi wa mabweni mawili (2) na vyumba viwili (2) vya madarasa katika Shule ya Sekondari Handeni,Ujenzi wa choo soko jipya la Seuta,Kikundi cha vijana cha deep c furniture kilichopo Kata ya Mabanda,na walengwa/wanufaika wa mradi wa TASAF ambapo kaya mbili (2) zilitembelewa.

Katika ziara hizo Waheshimiwa Madiwani wamefanikiwa kupata maelezo ya lini ujenzi wa Ofisi mpya za Halmashauri ya Mji Handeni litaanza kujengwa,na namna ambavyo Wakala wa Majengo Tanzania (TBA) ambao ndiyo wanahusika na ujenzi huo namna walivyojipanga kuhakikisha mradi huo unaenda kwa kasi inayotakiwa pamoja na ubora.

Aidha Kamati imepongeza ya ujenzi wa matundu ya vyoo katika Shule ya Msingi Kwakivesa kwa kazi nzuri waliyoifanya kwa kuhakikisha fedha waliyoipata inatumika ipasavyo kwa kuonyesha kazi imefanyika kwa kiwango kikubwa vilevile na nguvu kazi ya wanajamii imechangia kwa kiasi kikubwa mradi huo kwenda kwa kasi.

Vilvile Kamati ya fedha na utawala imepongeza kikundi cha vijana cha deep c furniture kilichopo Kata ya Mabanda kwa kundelea kuwa wabunifu kwa kutengeneza bidhaa mbalimbali zenye ubora na kukuza Soko lao ndani na nje ya Halmashauri ya Mji Handeni,Kikundi hiki kinatengeneza bidhaa kama majiko yenye ukubwa tofauti tofauti,Ovena za kuokea mikate na kuchoma nyama,na matranka kwa ajili ya wanafunzi.

Kwenye miradi ambayo Wananchi wanapaswa kushiriki nguvu kazi Kamati imeagiza viongozi wa Kata na Mitaa maeneo husika kuhakikisha wanahamasisha wananchi kujitokeza kwa wingi kushiriki kazi ambazo wanaweza kufanya ili kusaidia ukamilishwaji wa miradi kwa wakati,hasa ukizingatia miradi hiyo ni kwa ajili ya manufaa yao na jamii nzima inayozunguka eneo husika,hivyo wanaowajibu kuhakikisha wanashiriki kikamilifu na kumiliki mradi uliopo kwenye maeneo yao ili uweze kutunzwa vyema na wananchi wenyewe.



picha hapo juu zikionyesha wajumbe wakikagua na kupata maelezo kwenye eneo la ujenzi wa Ofisi mpya za Halmashauri


Mwenyekiti wa Halmashauri Mhe.Twaha Mgaya akishiriki zoezi la ujenzi wa matundu ya vyoo Shule ya Msingi Misima

Matangazo

  • KUITWA KWENYE USAILI 2 October 03, 2024
  • KUITWA KWENYE USAILI 1 September 27, 2024
  • TANGAZO LA MAJINA NA MIPAKA YA MITAA September 16, 2024
  • Angalia zaidi

Habari Mpya

  • HOSPITALI YA HALMASHAURI YA MJI HANDENI IMETOA ELIMU YA KUJINGA KWA MAGONJWA YA KUAMBUKIZA KWA WAFANYAKAZI WA BOMBA LA MAFUTA WILAYA YA HANDENI EACOP

    March 21, 2025
  • BARAZA MAALUMU LA MADIWANI LAPENDEKEZA KUONGEZEWA MAENEO YA UTAWALA

    March 14, 2025
  • MKUTANO MKUU WA 39 WA JUMUIYA YA TAWALA ZA MITAA TANZANIA (ALAT)

    March 11, 2025
  • ZIARA YA MHE. RAIS DKT SAMIA SULUHU HASSAN

    February 25, 2025
  • Angalia zaidi

Video

Mbunge wa jimbo la Handeni Mjini Mh.Reuben Kwagilwa aliamsha Bungeni
More Videos

Viunganishi vya Haraka

  • Dira na Dhamira
  • Kupata leseni ya Biashara
  • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
  • Kumuona Mkurugenzi
  • Kupata kibali cha Matangazo
  • Muundo wa Tasisi
  • Kumuona Mwenyekiti wa Halmashauri

Viunganishi Linganifu

  • Sekretariti ya Ajira
  • Ofisi ya Rais - Ikulu
  • FFARS-LIVE
  • PLANREP- BAJETI 2020/21
  • TAMISEMI
  • Utumishi

Watembeleaji wa Dunia

world map hits counter

Idadi ya waliotembelea tovuti

free HitCounter

Ramani

Wasiliana na sisi

    Barabara ya Korogwe - Handeni

    Anuani ya Posta: S.L.P 51 HANDENI

    Simu ya Mezani: 027-2641807

    Simu ya Mkononi:

    Barua pepe: td@handenitc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera za faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Copyright ©2022 GWF . All rights reserved.