• Wasiliana na sisi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Handeni Town Council
Handeni Town Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Mji Handeni

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Fedha na Biashara
      • Mipango,Takwimu na Ufuatiliaji
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo,Umwagiliaji na Ushirika
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Elimu Msingi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Maji
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Ardhi na Maliasili
      • Elimu Sekondari
      • Usafi na Mazingira
    • Vitengo
      • Teknolojia,Habari na Mawasiliano
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • Ugavi
      • Nyuki
      • Sheria
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya kitalii
    • kilimo
    • ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • fedha na uongozi
      • mipango miji na mazingira
      • uchumi afya na elimu
      • ukimwi
      • maadili
    • Ratiba
      • vikao vya waheshimiwa madiwani
      • kuonana na mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma Kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Miongozo Mbalimbali
    • fomu mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za Shughuli za Ofisi au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha
    • Matukio

Maadhimisho ya siku ya wanawake duniani yafana, Halmashauri ya Mji Handeni

Posted on: March 8th, 2023

Leo Tarehe 08/03/2023 Halmashauri ya Mji Handeni, imeadhimisha siku ya wanawake duniani yenye kauli mbiu ”UBUNIFU WA MABADILIKO YA TEKNOLOJIA:CHACHU KATIKA KULETA USAWA WA KIJINSIA”, katika kata ya  Konje, mtaa wa Konje shule, ghafla hiyo imehudhuriwa na viongozi mbalimbali wakiwemo mwenyekiti wa Halmashauri ya Mji Handeni, mkurugenzi wa Halmashauri ya Mji Handeni, waheshmiwa madiwani, watumishi kutoka Halmashauri ya Mji Handeni, wadau wa maendeleo ya jamii(CAMFED) na wananchi.

Mkurugenzi wa Halmashauri ya Mji Handeni Bi.Maryam Ukwaju na Mhe.Amina Kigoda Diwani viti maalum, wakijumuika na wananchi waliojitokeza katika kusherehekea maadhimisho ya siku ya wanawake duniani

Akizungumza katika hafla hiyo mwenyekiti wa Halmashauri(Diwani) wa kata ya Kwamagome Mhe.Mussa Mkombati ambaye ni mgeni rasmi, amempongeza mkurugenzi wa Halmashauri ya mji Handeni Bi.Maryam Ukwaju kwa namna anavyoweza kusimamia kama mtendaji mkuu wa Halmashauri, kwa kutenga fedha kwa ajili ya miradi ya maendeleo na fedha asilimia 10 kwa ajili ya mikopo ya kina mama, vijana na walemavu, pia amewataka walionufaika na mikopo wafanye marejesho kwa wakati ili wengine waendelee kunufaika na mikopo hiyo, Mhe.Mussa Mkombati aliendelea kwa kuwapa rai wakinamama wajitokeze Halmashauri ya mji Handeni na kuomba mikopo isiyo na riba na kuepuka kuchukua mikopo kwenye taasisi  zenye masharti magumu, pia amewasisitiza wazazi kuwapeleka watoto shule hasa watoto wa kike ambao wanaathirika sana na changamoto ya kutopelekwa shule, kwani kushindwa kuwasimamia watoto kupata haki zao ndio sababu inayopelekea uharibifu wa maadili na hatimaye mimba za utotoni.

Mwenyekiti wa Halmashauri ya Mji Handeni(Diwani) kata ya Kwamagome Mhe.Mussa Mkombati, akimzawadia  Mkurugenzi wa Halmashauri ya Mji Handeni Bi.Maryam Ukwaju kwa utendaji kazi wake uliotukuka, katika maadhimisho ya siku ya wanawake duniani 

Nae mkurugenzi wa Halmashauri ya Mji Handeni Bi.Maryam Ukwaju, akizungumza na wananchi waliojitokeza katika hafla hiyo, ameendelea kuwahamasisha wakina mama  wajiunge na  vikundi  ili kuweza kupata fursa ya mikopo inayotolewa na Halmashauri ya Mji Handeni, na pia amewashauri walionufaika na mikopo hiyo  watumie pesa hizo kwa malengo yaliyokusudiwa, ili kuweza kufanya marejesho kwa urahisi na kufikia malengo ya kujikwamua katika hali zao za kiuchumi, pia amewataka wazazi kutenga muda  wa kuwasimamia na kufuatilia mienendo ya watoto wao wakike na wakiume ili kukabiliana na uharibifu wa maadili unaotokea katika jamii.

Katika hafla hiyo Afisa Maendeleo ya jamii wa Halmashauri ya Mji Handeni, Ndugu.Fred Mpondachuma  amewasisitiza wazazi kuhakikisha watoto wote wanaostahili kupata elimu wanapelekwa shule ili waweze kupata haki yao ya msingi ya elimu, pia amewataka wakina baba wawapatie fursa wakina mama katika kushiriki masuala yote ya kijamii bila kuwaacha nyuma na kuthamini michango yao katika jamii, Ndugu.Fred Mpondachuma amewaasa wazazi kutowaozesha watoto wao waliokuwa na umri mdogo ili kudhibiti ndoa za utotoni ambazo zinamkwamisha mtoto wa kike kutimiza ndoto zake. Na amewataka wanakikundi kufuata taratibu zote ikiwa ni pamoja na kuwa na barua kutoka ofisi ya mtendaji pindi wanapofuatilia mikopo ili kuepusha kuchelewa kwa kupata mikopo hiyo.

Wadau wa maendeleo ya jamii Campaign for Female Education(CAMFED) wakitoa msaada kwa wanafunzi wa kike shule ya sekondari Konje, katika maadhimisho ya siku ya wanawake duniani yaliyofanyika Halmashauri ya Mji Handeni

Nae mkazi wa kata ya Konje Bi.Graciana Shirima, ametoa shukrani kwa Raisi wa Jamhuri ya muungano wa Tanzania Dokta.Samia Suluhu Hassan, kwa kuwajali na kuwapa kipaumbele wanawake hususani katika suala la mikopo wanayoipata, ambayo imeweza kuwasaidia watoto katika afya, elimu na mahitaji mbalimbali ya kila siku, pia ametumia fursa hiyo kuhamasisha wanawake ambao hawajachukua mikopo, kuwa mikopo hiyo inayotolewa na Halmashauri ya Mji Handeni, haina riba na ni haki yao hivyo wajitokeze kwenye fursa hiyo, na kutumia mikopo hiyo pindi wanapoipata kwa  lengo la kujikwamua kiuchumi.

Abdulkadir Kassim

Handeni Mji

Matangazo

  • TANGAZO LA KAZI UJENZI WA JENGO LA DHARURA (EMD) HOSPITALI YA WILAYA HANDENI February 16, 2023
  • Angalia zaidi

Habari Mpya

  • Afisa elimu msingi: Kula shuleni ni lazima

    March 13, 2023
  • Maadhimisho ya siku ya wanawake duniani yafana, Halmashauri ya Mji Handeni

    March 08, 2023
  • Walimu Halmashauri ya Mji Handeni, wapata mafunzo ya mfumo wa FFARS

    March 04, 2023
  • MILIONI 63.6 ZAMWAGWA KWA WAJASIRIAMALI HANDENI MJI. RAIS SAMIA ATAJWA.

    March 03, 2023
  • Angalia zaidi

Video

Mbunge wa jimbo la Handeni Mjini Mh.Reuben Kwagilwa aliamsha Bungeni
More Videos

Viunganishi vya Haraka

  • Dira na Dhamira
  • Kupata leseni ya Biashara
  • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
  • Kumuona Mkurugenzi
  • Kupata kibali cha Matangazo
  • Muundo wa Tasisi
  • Kumuona Mwenyekiti wa Halmashauri

Viunganishi Linganifu

  • Sekretariti ya Ajira
  • Ofisi ya Rais - Ikulu
  • FFARS-LIVE
  • PLANREP- BAJETI 2020/21
  • TAMISEMI
  • Utumishi

Watembeleaji wa Dunia

world map hits counter

Idadi ya waliotembelea tovuti

free HitCounter

Ramani

Wasiliana na sisi

    Barabara ya Korogwe - Handeni

    Anuani ya Posta: S.L.P 51 HANDENI

    Simu ya Mezani: 027-2641807

    Simu ya Mkononi:

    Barua pepe: td@handenitc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera za faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Copyright ©2022 GWF . All rights reserved.