• Wasiliana na sisi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Handeni Town Council
Handeni Town Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Mji Handeni

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Fedha na Biashara
      • Mipango,Takwimu na Ufuatiliaji
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo,Umwagiliaji na Ushirika
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Elimu Msingi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Maji
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Ardhi na Maliasili
      • Elimu Sekondari
      • Usafi na Mazingira
    • Vitengo
      • Teknolojia,Habari na Mawasiliano
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • Ugavi
      • Nyuki
      • Sheria
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya kitalii
    • kilimo
    • ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • fedha na uongozi
      • mipango miji na mazingira
      • uchumi afya na elimu
      • ukimwi
      • maadili
    • Ratiba
      • vikao vya waheshimiwa madiwani
      • kuonana na mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma Kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Miongozo Mbalimbali
    • fomu mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za Shughuli za Ofisi au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha
    • Matukio

MILIONI 63.6 ZAMWAGWA KWA WAJASIRIAMALI HANDENI MJI. RAIS SAMIA ATAJWA.

Posted on: March 3rd, 2023

Leo tarehe 03/03/2023 Halmashauri ya Mji Handeni imetoa jumla ya shilingi milioni 63,665,300 kwa vikundi vya wajasiriamali mbalimbali wa Halmashauri ya mji Handeni fedha zinazotakana na asilimia kumi ya mapato ya ndani katika ghafla fupi iliyofanyika katika eneo la Bomani, mahali ilipo ofisi ya Mkuu wa wilaya ya Handeni.

Akizungumza mbele ya Mgeni rasmi, Mkuu wa Idara ya Maendeleo ya Jamii Fred Mpondachuma alisema fedha hizo ni asilimia 10 ya mapato ya ndani ya Halmashauri ya mji Handeni katika robo ya pili ya mwaka wa fedha 2022/23 iliyoanza mwezi wa 10 hadi mwezi wa 12, ambapo mikopo hiyo ni maalumu kwa vijana, wanawake na watu wenye ulemavu huku akitaja jumla ya vikundi 18 vilivyoomba na kukidhi vigezo kunufaika na mkopo huo, amesema vikundi vya wanawake vipo 9, vikundi vya vijana vipo 6 na vikundi vya watu wenye ulemavu vipo 3. Bw. Mpondachuma amesema milioni 63 zilizotolewa mkopo siku ya leo zina mchanganuo ufuatao, milioni 42 zimetokana na 10% ya pato la ndani la Halmashauri na milioni 21 ni fedha zilizokusanywa kutoka kwenye marejesho ya waliokopeshwa hapo kabla.

Mkuu wa Idara ya maendeleo ya jamii Halmashauri ya Mji Handeni Ndugu. Fred Mpondachuma akikabidhi taarifa fupi kwa Katibu Tawala wilaya ya Handeni Mh. Mashaka Mgeta wakati wa ghafla ya ugawaji mikopo inayotokana na asilimia 10 ya mapato ya ndani.

Nae Mkurugenzi wa Halmashauri ya Mji Handeni, Bi.Maryam Ukwaju amemueleza mgeni rasmi kuwa mpaka kufikia sasa Halmashauri imeshatoa zaidi ya milioni mia moja na nne ikiwa ni asilimia 10 ya mapato ya ndani ya Halmashauri ya mji Handeni kwa ajili ya mikopo hiyo kwa vijana, wanawake na watu wenye ulemavu. Amesema, Halmashauri inaendelea kukusanya vizuri na mpaka kufikia mwishoni mwa mwaka huu wa fedha mwezi Juni 2023 Halmashauri itakuwa imefikia zaidi ya asilimia 100 katika utoaji wa mikopo hiyo.

Mkurugenzi wa Halmashauri ya Mji Handeni Bi. Maryam Ukwaju akizungumza mbele ya mgeni rasmi, hayupo pichani

Mgeni rasmi katika ghafla hiyo iliyohudhuriwa na viongozi mbalimbali wa chama na serikali, Mkuu wa wilaya ya Handeni Mh. Alberto Msando amewapongeza viongozi wa Halmashauri hiyo, Mwenyekiti Mh.Mussa Mkombati na Mkurugenzi wake Mh.Maryam Ukwaju kwa kutimiza ilani ya Chama cha Mapinduzi na pia wajibu huo wa kisheria. Amewahakikishia ya kwamba, atasimamia kikamilifu kuhakikisha uwezeshaji huu wa kiuchumi unakwenda kuwa na tija kwa kila mnufaika ili waweze kukua kiuchumi kwa haraka Zaidi. Amewatahadharisha wanufaika hao ya kwamba katika fedha walizokopeshwa, haitapotea hata shilingi moja katika kipindi chote atakachohudumu katika nafasi ya Mkuu wa wilaya ya Handeni, hivyo basi endapo kuna mtu amejiunga kwenye kikundi akifikiri mara baada yakukabidhiwa mkopo atakwamisha wengine kufanya marejesho, basi ni vyema akajitoa mapema kwenye kikundi hicho. Amewasihi wanakikundi, kusimamia katiba yao, kutunza amani na kuepuka mivurugano itakayopelekea wao kushindwa kutimiza lengo la kuchukua mkopo huo. Kwa upande wa waliochukua mkopo wa vyombo vya usafiri, amewataka kuzingatia sheria za barabarani ili kuepuka kukamatwa na pikipiki kuzuiliwa hali itakayopelekea kushindwa kurejesha mkopo kwa wakati na kujiondolea sifa za kuendelea kukopesheka.

Wanufaika wa mikopo Halmashauri ya mji Handeni wakimsikiliza mgeni rasmi Mh. Alberto Msando, Mkuu wa wilaya ya Handeni.

Akizungumza mara baada ya kupokea mkopo kwa niaba ya wanakikundi wengine waliopokea mkopo wa pikipiki, mwanakikundi Ibrahim Mrisho Bakari dereva bodaboda wa Kata ya Chanika, amesema wamepokea mkopo huo kwa furaha sana, na wanamshukuru Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan kwasababu pikipiki walizokopeshwa zitawasaidia kujikwamua kiuchumi na kuwasogeza mbele kimaisha kwani bodaboda ni ajira halali na inaingiza kipato kinachowafanya wakidhi mahitaji yao ya kila siku, aidha Bwana Ibrahim ametoa wito kwa wananchi wote wenye sifa kujitokeza na kuchangamkia fursa kwenye Halmashauri zao ili waweze kupatiwa mikopo hiyo.

Mkuu wa wilaya ya Handeni Mh. Alberto Msando akimkabidhi Bajaji Bw.Mhina Omari Mahimbo katika ghafla ya utoaji mikopo

Nae Bw.Mhina Omari Mahimbo aliyepatiwa mkopo wa pikipiki ya magurudumu matatu maarufu Bajaji, akizungumza kwa niaba ya watu wenye ulemavu waliopatiwa mikopo mbalimbali katika ghafla hiyo amesema mwanzoni hakua akijua kuwa watu wenye ulemavu wanaweza wakakopeshwa na serikali, lakini kupitia matangazo mbalimbali na hamasa iliyokuwa ikifanywa na Mkurugenzi wa Halmashauri ya Mji Handeni Bi. Maryam Ukwaju aliweza kuhamasika na kufika ofisi za Halmashauri ambapo aliweza kupewa utaratibu ambao ulikuwa rahisi, usio na konakona yoyote na mara baada ya kukamilisha taratibu hizo amefurahi leo kukabidhiwa Bajaji yake. Ameahidi ya kwamba ataitunza vyema, na kutoa ajira kwa mtu mmoja atakaye endesha Bajaji hiyo na kumuingizia kipato ili aweze kurejesha mkopo huo na kuchukua mwingine.

Abdulkadir Kassim

Handeni Mji

Matangazo

  • TANGAZO LA KAZI UJENZI WA JENGO LA DHARURA (EMD) HOSPITALI YA WILAYA HANDENI February 16, 2023
  • Angalia zaidi

Habari Mpya

  • Afisa elimu msingi: Kula shuleni ni lazima

    March 13, 2023
  • Maadhimisho ya siku ya wanawake duniani yafana, Halmashauri ya Mji Handeni

    March 08, 2023
  • Walimu Halmashauri ya Mji Handeni, wapata mafunzo ya mfumo wa FFARS

    March 04, 2023
  • MILIONI 63.6 ZAMWAGWA KWA WAJASIRIAMALI HANDENI MJI. RAIS SAMIA ATAJWA.

    March 03, 2023
  • Angalia zaidi

Video

Mbunge wa jimbo la Handeni Mjini Mh.Reuben Kwagilwa aliamsha Bungeni
More Videos

Viunganishi vya Haraka

  • Dira na Dhamira
  • Kupata leseni ya Biashara
  • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
  • Kumuona Mkurugenzi
  • Kupata kibali cha Matangazo
  • Muundo wa Tasisi
  • Kumuona Mwenyekiti wa Halmashauri

Viunganishi Linganifu

  • Sekretariti ya Ajira
  • Ofisi ya Rais - Ikulu
  • FFARS-LIVE
  • PLANREP- BAJETI 2020/21
  • TAMISEMI
  • Utumishi

Watembeleaji wa Dunia

world map hits counter

Idadi ya waliotembelea tovuti

free HitCounter

Ramani

Wasiliana na sisi

    Barabara ya Korogwe - Handeni

    Anuani ya Posta: S.L.P 51 HANDENI

    Simu ya Mezani: 027-2641807

    Simu ya Mkononi:

    Barua pepe: td@handenitc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera za faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Copyright ©2022 GWF . All rights reserved.