• Wasiliana na sisi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Handeni Town Council
Handeni Town Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Mji Handeni

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Fedha na Biashara
      • Mipango,Takwimu na Ufuatiliaji
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo,Umwagiliaji na Ushirika
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Elimu Msingi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Maji
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Ardhi na Maliasili
      • Elimu Sekondari
      • Usafi na Mazingira
    • Vitengo
      • Teknolojia,Habari na Mawasiliano
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • Ugavi
      • Nyuki
      • Sheria
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya kitalii
    • kilimo
    • ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • fedha na uongozi
      • mipango miji na mazingira
      • uchumi afya na elimu
      • ukimwi
      • maadili
    • Ratiba
      • vikao vya waheshimiwa madiwani
      • kuonana na mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma Kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Miongozo Mbalimbali
    • fomu mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za Shughuli za Ofisi au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha
    • Matukio

Mkuu wa mkoa wa Tanga afanya ziara ya siku mbili Halmashauri ya Mji Handeni

Posted on: November 3rd, 2022

Leo Alhamisi, tarehe 3 Novemba 2022 Mkuu wa mkoa wa Tanga Mh.Omari Tebweta Mgumba amehitimisha ziara ya siku mbili katika Halmashauri ya Mji Handeni aliyoianza tarehe 2 Novemba 2022 siku ya Jumatano. Katika ziara hiyo Mheshimiwa mkuu wa mkoa akiambatana na mwenyeji wake Mkuu wa wilaya ya Handeni Mh.Siriel Mchembe ametembelea jumla ya miradi saba ya maendeleo na kufanya mikutano mitatu ya hadhara na wananchi wa Handeni Mjini.

Katika ziara hiyo Mh.Omari Mgumba alitembelea miradi ya maendeleo ifuatayo, kituo namba 15 cha mradi wa bomba la mafuta ghafi la Afrika Mashariki(EACOP) unaotokea Kabaale-Hoima nchini Uganda kwenda kwenye peninsula ya Chongoleani mkoani Tanga nchini Tanzania unaojengwa katika kata ya Mabanda Halmashauri ya Mji Handeni na mkandarasi mzawa kampuni ya SPEK, pia alitembelea ujenzi wa maabara za shule ya sekondari Misima kata ya Mabanda, ujenzi wa shule mpya ya msingi Bondo kata ya Kwamagome, ujenzi wa shule mpya ya sekondari Togeza kata ya Kwamagome. Miradi mingine aliyotembelea ni pamoja na ujenzi wa shule mpya ya sekondari Mlimani kata ya Mlimani, ujenzi wa kituo kipya cha afya Malezi kata ya Malezi na ujenzi wa shule mpya ya sekondari Mapinduzi kata ya Kwenjugo.

Akizungumza katika nyakati tofauti Mh.Omari Mgumba alishukuru, alipongeza, alielekeza na pia aliagiza mambo mbalimbali katika kuongeza ufanisi wa utoaji huduma wa serikali kwenda kwa wananchi, ambapo katika mradi wa ujenzi wa bomba la mafuta alimshukuru mkandarasi kwa kuzingatia vigezo vya kitaifa na kimataifa vya uthaminishaji na utoaji fidia kwa wananchi walioondoka kwenye maeneo yao ili kupisha utekelezaji wa mradi huo, nae mkandarasi anaesimamia ujenzi huo Mhandisi Alnord Sililo alimueleza mkuu wa Mkoa ya kwamba mradi umefikia 48% na unatarajiwa kukamilika ifikapo tarehe 22 Disemba 2022, alieleza pia wakazi wa Mabanda na Misima wamenufaika  moja kwa moja kutokana na ujenzi huo mahali hapo kwa kutatua changamoto ya uhaba wa maji ambapo visima viwili vya mradi huo vimekuwa vikihudumia wakazi wa eneo hilo na kuahidi kuwa mara baada ya mradi huo kukamilika visima hivyo vitakabidhiwa serikalini ili kuendelea kuwanufaisha wananchi wa maeneo hayo na maeneo ya jirani, vilevile watapatiwa mashamba mapya na kuelekezwa namna ya kulima kisasa.

Aidha Mh.Omari Mgumba alipotembela katika ujenzi wa maabara za shule ya sekondari Misima alipongeza baada ya kuridhishwa na hali ya mradi huo na kuwataka wanafunzi wa shule hiyo kuendelea kusoma kwa bidii, pia alielekeza ujenzi wa uzio utakaounganisha jengo la bweni na vyoo vya wasichana ili kuimarisha usalama wa matumizi wa vyoo hivyo hususani kipindi cha usiku ambapo inawalazimu wanafunzi hao kushindwa kutumia vyoo hivyo ipasavyo kwa kuhofia usalama wao.

Akiwahutubia wananchi wa Bondo mtaa wa Kwaluwala, kata ya Kwamagome, Mheshimiwa mkuu wa mkoa amewapongeza wananchi hao kwa kujitoa kwao katika kujiletea maendeleo kwa kushirikiana na serikali katika ujenzi wa shule mpya ya msingi Bondo. Wakati huohuo amewasihi wakazi wa eneo hilo kuendelea kuvuta subira wakati serikali ikiendelea kufanyia kazi suala la mgogoro wa mipaka kati ya halmashauri ya Mji Handeni na halmashauri ya wilaya ya Kilindi ili kubaini eneo hilo kiutawala liko wapi, huku pia kukiwepo na taarifa inayosema eneo hilo ni msitu unaomilikiwa kihalali na Wakala wa Misitu Tanzania(TFS). Mheshimiwa mkuu wa mkoa amewaahidi wananchi hao mpaka kufikia tarehe 4 Novemba 2022 muafaka wa utatuzi wa migogoro hiyo utapatikana na watafahamishwa.

Katika ziara yake Mh. Omari Mgumba alitembelea ujenzi wa shule mpya ya sekondari Mlimani na kuvutiwa na ubora wa majengo ya shule hiyo, hata hivyo amemuagiza  Mhandisi wa halmashauri ya Mji Handeni, Benny Komba kukamilisha ujenzi huo kwa kufanya kazi usiku na mchana kwani licha ya ubora wa majengo hayo lakini ujenzi upo nyuma ya muda na ukamilike ndani ya wiki mbili na pia ameagiza kukamilisha utengenezaji wa thamani  (meza na viti) vya shule hiyo kwa idadi iliyotolewa katika muongozo  na kwa bajeti ya mradi huo.

Akiwa katika kituo kipya cha afya Malezi, Mheshimiwa mkuu wa mkoa ametoa pongezi juu ya hatua iliyofikiwa ya ujenzi na kuanza kutumika kwa kituo hicho kitakachoondoa adha ya wananchi kutembea umbali mrefu kwa ajili ya kupata huduma za afya ikiwemo kliniki ya mama na mtoto. Halikadhalika kituo hicho kinakwenda kuongeza idadi ya ajira mpya kwenye kada ya afya na nyinginezo.

Alipotembelea kata ya Kwenjugo mahali panapotekelezwa ujenzi wa shule mpya ya sekondari Mapinduzi kwa nguvu za wananchi Mheshimiwa mkuu wa mkoa ameagiza ujenzi wa shule hiyo uliokuwa unatekelezwa bila ya kufuata utaratibu uliowekwa na Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa(TAMISEMI) usimame mara moja mpaka taratibu zitakapofuatwa kikamilifu.

Mheshimiwa mkuu wa mkoa alihitimisha ziara hiyo kwa kufanya mkutano wa hadhara na wananchi wa Mji wa Handeni katika mtaa wa Vibaoni, kata ya Vibaoni ambapo wananchi walipata fursa ya kumshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mh.Samia Suluhu Hassan kwa kuelekeza fedha za miradi mbalimbali katika Halmashauri yao na kumuomba Mkuu wa Mkoa kufikisha shukrani zao za dhati kwa mheshimiwa Rais, pia walipata nafasi ya kuuliza maswali mbalimbali, yaliyotolewa majibu na mheshimiwa mkuu wa mkoa, mkuu wa wilaya, mwenyekiti wa halmashauri Mh. Mussa Mkombati(Diwani CCM) na mkurugenzi wa halmashauri ya Mji Handeni, Mh. Maryam Ukwaju.

Kwa upande wake Mkurugenzi wa Halmashauri ya mji Handeni Bi.Maryam Ukwaju amesema amepokea maelekezo yote yaliyotolewa na Mkuu wa Mkoa kwa kuahidi kuanza kuyafanyia kazi mara moja. 

Mheshimiwa mkuu wa Mkoa amehitimisha ziara yake kwa kuwapongeza viongozi wa chama na serikali, vyombo vya ulinzi na usalama, pamoja na wananchi wa halmashauri ya Mji Handeni, kwa kudumisha amani na kutoa ushirikiano kikamilifu katika ziara yake ya kikazi ya muda wa siku mbili.


Abdulkadir Kassim

Handeni Mji

Matangazo

  • KUITWA KWENYE USAILI 2 October 03, 2024
  • KUITWA KWENYE USAILI 1 September 27, 2024
  • TANGAZO LA MAJINA NA MIPAKA YA MITAA September 16, 2024
  • Angalia zaidi

Habari Mpya

  • HOSPITALI YA HALMASHAURI YA MJI HANDENI IMETOA ELIMU YA KUJINGA KWA MAGONJWA YA KUAMBUKIZA KWA WAFANYAKAZI WA BOMBA LA MAFUTA WILAYA YA HANDENI EACOP

    March 21, 2025
  • BARAZA MAALUMU LA MADIWANI LAPENDEKEZA KUONGEZEWA MAENEO YA UTAWALA

    March 14, 2025
  • MKUTANO MKUU WA 39 WA JUMUIYA YA TAWALA ZA MITAA TANZANIA (ALAT)

    March 11, 2025
  • ZIARA YA MHE. RAIS DKT SAMIA SULUHU HASSAN

    February 25, 2025
  • Angalia zaidi

Video

Mbunge wa jimbo la Handeni Mjini Mh.Reuben Kwagilwa aliamsha Bungeni
More Videos

Viunganishi vya Haraka

  • Dira na Dhamira
  • Kupata leseni ya Biashara
  • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
  • Kumuona Mkurugenzi
  • Kupata kibali cha Matangazo
  • Muundo wa Tasisi
  • Kumuona Mwenyekiti wa Halmashauri

Viunganishi Linganifu

  • Sekretariti ya Ajira
  • Ofisi ya Rais - Ikulu
  • FFARS-LIVE
  • PLANREP- BAJETI 2020/21
  • TAMISEMI
  • Utumishi

Watembeleaji wa Dunia

world map hits counter

Idadi ya waliotembelea tovuti

free HitCounter

Ramani

Wasiliana na sisi

    Barabara ya Korogwe - Handeni

    Anuani ya Posta: S.L.P 51 HANDENI

    Simu ya Mezani: 027-2641807

    Simu ya Mkononi:

    Barua pepe: td@handenitc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera za faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Copyright ©2022 GWF . All rights reserved.