• Wasiliana na sisi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Handeni Town Council
Handeni Town Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Mji Handeni

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Fedha na Biashara
      • Mipango,Takwimu na Ufuatiliaji
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo,Umwagiliaji na Ushirika
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Elimu Msingi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Maji
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Ardhi na Maliasili
      • Elimu Sekondari
      • Usafi na Mazingira
    • Vitengo
      • Teknolojia,Habari na Mawasiliano
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • Ugavi
      • Nyuki
      • Sheria
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya kitalii
    • kilimo
    • ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • fedha na uongozi
      • mipango miji na mazingira
      • uchumi afya na elimu
      • ukimwi
      • maadili
    • Ratiba
      • vikao vya waheshimiwa madiwani
      • kuonana na mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma Kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Miongozo Mbalimbali
    • fomu mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za Shughuli za Ofisi au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha
    • Matukio

MKUU WA WILAYA, MKURUGENZI HANDENI MJI WAWAONGOZA WANANCHI KUPIMA KWA HIARI SIKU YA UKIMWI DUNIANI

Posted on: December 1st, 2022

Leo Alhamisi, tarehe 1 Desemba 2022 maadhimisho ya siku ya UKIMWI yamefanyika katika kituo cha Afya Malezi kilichopo Halmashauri ya Mji Handeni kata ya Malezi. Viongozi mbalimbali pamoja na wananchi wamehudhuria katika maadhimisho hayo ambapo mgeni rasmi alikuwa ni Mheshimiwa Mkuu wa Wilaya Bi.Siriel Mchembe.Katika maadhimisho hayo viongozi pamoja na wananchi wamejitokeza kupima kwa hiari VVU, kutambua hali zao za kiafya na kutoa ushirikiano wa juhudi za serikali na wadau mbalimbali wa masuala ya UKIMWI.

Katika maadhimisho hayo Mkuu wa Wilaya ya Handeni Bi.Siriel Mchembe amewataka wananchi kuchukua tahadhari kutokana na matumizi ya pamoja kwa vitu vyenye ncha kali hususani kwenye maeneo wanapopata huduma za saloon kwani vifaa vinavyotumika kutolea huduma ni vyenye ncha kali hivyo visipotumika ipasavyo na kutochemshwa vitapelekea kuongezeka kwa maambukizi mapya ya virusi vya UKIMWI .

Wakati huohuo mwenyekiti wa Halmashauri ya Mji Handeni Mh.Mussa Mkombati(Diwani CCM) amewataka wananchi kujitokeza kupima virusi vya UKIMWI pale wanapopata nafasi ya kufanya hivyo na kuwahakikishia kuwa huduma hii inapatikana kwa wakati kwa kila anayestahili.

Nae Mkurugenzi wa Halmashauri ya Mji Handeni, Bi.Maryam Ukwaju amewataka wananchi kushirikiana na kutowanyanyapaa waathirika wa VVU na pia walioathirika wasijinyanyapae ili kuweka usawa katika jamii kwani kutambua Afya yako ni namna nzuri ya kuweza kuishi kwa matumaini na kutimiza malengo yako.

Akizungumza mbele ya mgeni rasmi, mratibu wa UKIMWI Halmashauri ya Mji Handeni Bi.Joyce Gidion amesema maambukizi ya VVU katika Halmashauri ya Mji Handeni yamepungua ambapo mpaka kufikia Oktoba 2022 idadi ya waliojitokeza kupima VVU ni jumla ya wananchi 9,453 kati yao wanaume ni 4,447 na wanawake ni 5,006 na kugundua walioathirika kuwa na idadi ya 365 wanaume wakiwa ni 164 sawa na 4% na wanawake ni 201 sawa na 3.7% ameeleza pia jumla ya wateja 2,600 wamepatiwa dawa za kufubaza VVU, 830 wakiwa ni wanaume na 1,770 ni wanawake.

Katika nyakati tofauti wananchi wameeleza changamoto zinazowapelekea kutojitokeza kwenye upimaji wa VVU moja wapo ni baadhi ya wananchi katika jamii kunyanyapaa waathirika wa VVU na kupelekea ukosefu wa usawa katika jamii, pia wameishukuru serikali na wadau mbalimbali wa masuala ya UKIMWI kwa jitihada za kutokomeza maambukizi mapya ya VVU kwa kuwapatia elimu kuhusu VVU katika vituo vya kutolea huduma za Afya, kinga za kuzuia maambukizi mapya na kutoa dawa kwa waathirika wa VVU.  

Abdulkadir Kassim

Handeni Mji

Matangazo

  • TOA MAONI/MALALAMIKO KATIKA OFISI ZA HALMASHAURI May 28, 2023
  • TANGAZO LA KAZI UJENZI WA JENGO LA DHARURA (EMD) HOSPITALI YA WILAYA HANDENI February 16, 2023
  • Angalia zaidi

Habari Mpya

  • Mradi wa Ujenzi wa Bwawa la Kwamaizi wakamilika

    July 14, 2023
  • WIKI YA MAPATO HANDENI MJI DC Msando ataja vyanzo vipya vya kukusanya mapato

    July 11, 2023
  • TUMEPOKEA GARI MPYA Kwa matumizi ya Idara ya Elimu Sekondari

    July 06, 2023
  • SIKUKUU YA EID EL ADHA Taasisi ya Islamic Help yatoa ng'ombe 1600 HANDENI

    June 30, 2023
  • Angalia zaidi

Video

Mbunge wa jimbo la Handeni Mjini Mh.Reuben Kwagilwa aliamsha Bungeni
More Videos

Viunganishi vya Haraka

  • Dira na Dhamira
  • Kupata leseni ya Biashara
  • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
  • Kumuona Mkurugenzi
  • Kupata kibali cha Matangazo
  • Muundo wa Tasisi
  • Kumuona Mwenyekiti wa Halmashauri

Viunganishi Linganifu

  • Sekretariti ya Ajira
  • Ofisi ya Rais - Ikulu
  • FFARS-LIVE
  • PLANREP- BAJETI 2020/21
  • TAMISEMI
  • Utumishi

Watembeleaji wa Dunia

world map hits counter

Idadi ya waliotembelea tovuti

free HitCounter

Ramani

Wasiliana na sisi

    Barabara ya Korogwe - Handeni

    Anuani ya Posta: S.L.P 51 HANDENI

    Simu ya Mezani: 027-2641807

    Simu ya Mkononi:

    Barua pepe: td@handenitc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera za faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Copyright ©2022 GWF . All rights reserved.