• Wasiliana na sisi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Handeni Town Council
Handeni Town Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Mji Handeni

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Fedha na Biashara
      • Mipango,Takwimu na Ufuatiliaji
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo,Umwagiliaji na Ushirika
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Elimu Msingi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Maji
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Ardhi na Maliasili
      • Elimu Sekondari
      • Usafi na Mazingira
    • Vitengo
      • Teknolojia,Habari na Mawasiliano
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • Ugavi
      • Nyuki
      • Sheria
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya kitalii
    • kilimo
    • ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • fedha na uongozi
      • mipango miji na mazingira
      • uchumi afya na elimu
      • ukimwi
      • maadili
    • Ratiba
      • vikao vya waheshimiwa madiwani
      • kuonana na mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma Kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Miongozo Mbalimbali
    • fomu mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za Shughuli za Ofisi au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha
    • Matukio

Mkuu wa wilaya ya Handeni agawa pembejeo na viuatilifu

Posted on: October 31st, 2022

Mkuu wa wilaya ya Handeni Bi.Siriel Mchembe ameongoza zoezi la ugawaji wa pembejeo na viuatilifu vya kilimo cha zao la korosho katika kata ya Vibaoni Mtaa wa Vibaoni Kati Halmashauri ya mji Handeni kwenye moja ya shamba la mfugaji na mkulima wa korosho Dkt.Raynold Mlinga.

Aidha kwenye zoezi hilo amemuagiza Afisa Kilimo kuunda mara moja AMCOS ili wakulima wapate soko na bei ya kueleweka ya zao la korosho ili kuepusha wakulima kuuza mazao yao kwa wanunuzi binafsi(vishoka) wa zao hilo la korosho na kupata adha ya kufuata soko la korosho (AMCOS) lililopo Mkata badala ya soko kumfuata mkulima kwa ajili ya manunuzi.

Pia Mh. Mkuu wa wilaya amemuagiza Mkurugenzi wa Halmashauri ya Mji Handeni Bi. Maryam Ukwaju kuhakikisha kuwa maafisa ugani wanakuwa na jukumu moja tu mbali na kukaimu katika nafasi nyengine za utendaji wa mitaa, lengo likiwa kuimarisha na kufikia  maendeleo ya zao la kimkakati la korosho kwa kuweza kupata muda mrefu kwa ajili ya kuwahudumia na kushirikiana na wakulima katika maeneo yao husika na kuepusha kukosekana huduma ya maafisa hao pindi panapokuwa na majukumu mengine ya kiutendaji.

Vilevile amemuagiza Afisa Kilimo  pamoja na kila afisa ugani kuwa na shamba darasa kwa ajili ya kuelimisha wakulima na kuwaonyesha namna bora juu ya kilimo cha zao hilo, kuhamasisha wakulima juu ya zao la korosho na namna linavyoweza kuinua hali ya kiuchumi ya mkulima, kugundua changamoto zitokanazo na wadudu na upungufu wa pembejeo na kutambua mazao yenye ustawi mzuri katika eneo hilo kwa kupanda aina tofauti za mazao ili kuwaelekeza namna bora ya kilimo cha zao hilo.

Katika zoezi hilo Mkuu wa Wilaya ya Handeni Bi.Siriel Mchembe amewataka wakulima wote  wajisajili katika daftari la wakulima katika mfumo wa kielektroniki ili wapate nafasi yakutambulika, kuelimishwa na kusaidiwa katika mbinu bora za kilimo.

Wakati huohuo amempongeza Afisa Kilimo wa Halmashauri ya Mji Handeni, Bi Aldegunda Matunda kwa kuweza kuongeza idadi ya miche ya zao hilo la kimkakati na kufikia idadi ya miche elfu kumi na tano(15,000) na kuweka malengo ya uzalishaji wa korosho kutoka tani 2.2 hadi tani 15.3 sawa na hekari 308 hadi hekari 1080 kwa mwaka wa kilimo 2022/23 na kumtaka asimamie utekelezaji wa malengo hayo, pia  amewasisitiza wakulima kupanda miche mingi zaidi ya zao la korosho ili kuweza kuepukana na mashamba pori.

Mkuu wa wilaya ya Handeni Bi.Siriel Mchembe ametumia nafasi hiyo kumpongeza Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mh.Samia Suluhu Hassan kwa kuongeza bajeti ya Sekta ya Kilimo  na kuipa nguvu maradufu ili kupiga vita maadui watatu  wa taifa yaani ujinga, umaskini na maradhi ambapo mkulima akiinuka kiuchumi ataweza kuepukana na umasikini, maradhi kwa kukata bima ya afya itakayompatia matibabu na ataweza kusomesha watoto ili waepukane  na ujinga.

Abdulkadir Kassim

Handeni Mji

Matangazo

  • KUITWA KWENYE USAILI 2 October 03, 2024
  • KUITWA KWENYE USAILI 1 September 27, 2024
  • TANGAZO LA MAJINA NA MIPAKA YA MITAA September 16, 2024
  • Angalia zaidi

Habari Mpya

  • HOSPITALI YA HALMASHAURI YA MJI HANDENI IMETOA ELIMU YA KUJINGA KWA MAGONJWA YA KUAMBUKIZA KWA WAFANYAKAZI WA BOMBA LA MAFUTA WILAYA YA HANDENI EACOP

    March 21, 2025
  • BARAZA MAALUMU LA MADIWANI LAPENDEKEZA KUONGEZEWA MAENEO YA UTAWALA

    March 14, 2025
  • MKUTANO MKUU WA 39 WA JUMUIYA YA TAWALA ZA MITAA TANZANIA (ALAT)

    March 11, 2025
  • ZIARA YA MHE. RAIS DKT SAMIA SULUHU HASSAN

    February 25, 2025
  • Angalia zaidi

Video

Mbunge wa jimbo la Handeni Mjini Mh.Reuben Kwagilwa aliamsha Bungeni
More Videos

Viunganishi vya Haraka

  • Dira na Dhamira
  • Kupata leseni ya Biashara
  • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
  • Kumuona Mkurugenzi
  • Kupata kibali cha Matangazo
  • Muundo wa Tasisi
  • Kumuona Mwenyekiti wa Halmashauri

Viunganishi Linganifu

  • Sekretariti ya Ajira
  • Ofisi ya Rais - Ikulu
  • FFARS-LIVE
  • PLANREP- BAJETI 2020/21
  • TAMISEMI
  • Utumishi

Watembeleaji wa Dunia

world map hits counter

Idadi ya waliotembelea tovuti

free HitCounter

Ramani

Wasiliana na sisi

    Barabara ya Korogwe - Handeni

    Anuani ya Posta: S.L.P 51 HANDENI

    Simu ya Mezani: 027-2641807

    Simu ya Mkononi:

    Barua pepe: td@handenitc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera za faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Copyright ©2022 GWF . All rights reserved.