• Wasiliana na sisi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Handeni Town Council
Handeni Town Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Mji Handeni

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Fedha na Biashara
      • Mipango,Takwimu na Ufuatiliaji
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo,Umwagiliaji na Ushirika
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Elimu Msingi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Maji
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Ardhi na Maliasili
      • Elimu Sekondari
      • Usafi na Mazingira
    • Vitengo
      • Teknolojia,Habari na Mawasiliano
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • Ugavi
      • Nyuki
      • Sheria
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya kitalii
    • kilimo
    • ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • fedha na uongozi
      • mipango miji na mazingira
      • uchumi afya na elimu
      • ukimwi
      • maadili
    • Ratiba
      • vikao vya waheshimiwa madiwani
      • kuonana na mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma Kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Miongozo Mbalimbali
    • fomu mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za Shughuli za Ofisi au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha
    • Matukio

Mradi wa Ujenzi wa Bwawa la Kwamaizi wakamilika

Posted on: July 14th, 2023

Leo Ijumaa ya tarehe 14 Julai 2023, Shirika la WaterAid Tanzania limeikabidhi Mamlaka ya Majisafi na Usafi wa Mazingira(HTM) bwawa la Maji, lilokuwepo Halmashauri ya Mji Handeni, mtaa wa Kampene katika kata ya Kideleko. Hafla ya makabidhiano hayo imehudhuriwa na Mgeni rasmi ambaye ni Naibu Waziri wa Maji Mhe.Maryprisca Mahundi.

Akizungumza katika hafla hiyo Mhe.Maryprisca Mahundi, amemshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt.Samia Suluhu Hassan, kwa jitihada anazozifanya katika kuboresha sekta ya maji katika Mkoa wa Tanga na Tanzania kwa ujumla. Vilevile amempongeza Mkuu wa wilaya  Mhe.Alberto Msando kwa Kushirikiana na Mamlaka ya maji vijijini(RUWASA) katika kusimamia utekelezaji wa mradi huo. Pia amempongeza Mbunge wa Jimbo la Handeni Mji Mhe.Reuben Kwagilwa kwa kutafuta wafadhili ambao wamekuja kuleta tija katika kuwezesha jamii kupata huduma karibu na makazi yao.

Mhe.Maryprisca Mahundi, ameishukuru kampuni ya Serengeti Breweries(SBL) kwa kufadhili mradi huo kwa fedha za Tanzania shilingi milioni 380 ambazo ni zaidi ya asilimia tisini (90%) za gharama ya mradi huo, ambao umesimamiwa na shirika la WaterAid.

Mkurugenzi mkazi wa shirika la WaterAid Tanzania Bi. Anna Mzinga, akisoma ripoti ya utekelezaji wa Mradi wa Bwawa la Kwamaizi mbele ya mgeni rasmi. Pichani wa pili kushoto ni Mhe.Maryprisca Mahundi Naibu Waziri wa maji, wa kwanza kushoto Mkuu wa wilaya ya Handeni Mh. Alberto Msando, Mbunge wa Handeni Mji Mhe.Reuben Kwagilwa wa Pili kulia na Mkurugenzi wa Halmashauri Bi.Maryam Ukwaju wa kwanza kulia 

 Nae Mkuu wa Wilaya ya Handeni Mhe.Alberto Msando amemshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kuwezesha upatikanaji wa maji katika wilaya ya Handeni kufika 40.6% kutoka asilimia 38% kama ilivyokuwa katika mwaka 2020/21, kwa kipindi kifupi alichokuwa madarakani. Ambapo Halmashauri ya Mji Handeni imekuwa na 42% za upatikanaji wa maji. Pia Mkuu wa wilaya ameahidi kuwa hakutakuwa na shilingi itakayopotea katika utekelezaji wa miradi , ili kuhakikisha miradi inakamilika kwa wakati na kuhakikisha upatikanaji wa maji safi na salama katika jamii kwa zaidi ya 85% kabla ya mwaka 2025.

Mkurugenzi wa Halmashauri ya Mji Handeni Bi.Maryam Ukwaju, akipokea cheti cha kutambuliwa kutoka kwa Naibu waziri wa Maji Mhe.Maryprisca Mahundi, kilichotolewa na Shirika la bia la Serengeti(SBL), katika hafla ya kukabidhi Bwawa la Kwamaizi kwa Mamlaka ya Majisafi na Usafi wa Mazingira(HTM)

Mhe.Reuben Kwagilwa ameishukuru Serikali ya awamu ya sita kwa kuunga mkono juhudi zinazofanywa na wadau mbalimbali wa maendeleo, ambapo wameweza kuleta mitambo kwenye utekelezaji wa mradi huo na kupunguza gharama ambazo zingehitajika kwa ajili ya kukodisha mitambo hiyo, Mhe.Kwagilwa amewataka wananchi kutunza mazingira na vyanzo vya maji pamoja na mradi huo, kwa kutofanya shughuli za makazi na uchumi kwa umbali wa mita 60 kutoka kwenye bwawa hilo, kwa kuwa mradi huo umetekelezwa kwa kuzingatia sheria za maji.

Matangazo

  • KUITWA KWENYE USAILI 2 October 03, 2024
  • KUITWA KWENYE USAILI 1 September 27, 2024
  • TANGAZO LA MAJINA NA MIPAKA YA MITAA September 16, 2024
  • Angalia zaidi

Habari Mpya

  • HOSPITALI YA HALMASHAURI YA MJI HANDENI IMETOA ELIMU YA KUJINGA KWA MAGONJWA YA KUAMBUKIZA KWA WAFANYAKAZI WA BOMBA LA MAFUTA WILAYA YA HANDENI EACOP

    March 21, 2025
  • BARAZA MAALUMU LA MADIWANI LAPENDEKEZA KUONGEZEWA MAENEO YA UTAWALA

    March 14, 2025
  • MKUTANO MKUU WA 39 WA JUMUIYA YA TAWALA ZA MITAA TANZANIA (ALAT)

    March 11, 2025
  • ZIARA YA MHE. RAIS DKT SAMIA SULUHU HASSAN

    February 25, 2025
  • Angalia zaidi

Video

Mbunge wa jimbo la Handeni Mjini Mh.Reuben Kwagilwa aliamsha Bungeni
More Videos

Viunganishi vya Haraka

  • Dira na Dhamira
  • Kupata leseni ya Biashara
  • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
  • Kumuona Mkurugenzi
  • Kupata kibali cha Matangazo
  • Muundo wa Tasisi
  • Kumuona Mwenyekiti wa Halmashauri

Viunganishi Linganifu

  • Sekretariti ya Ajira
  • Ofisi ya Rais - Ikulu
  • FFARS-LIVE
  • PLANREP- BAJETI 2020/21
  • TAMISEMI
  • Utumishi

Watembeleaji wa Dunia

world map hits counter

Idadi ya waliotembelea tovuti

free HitCounter

Ramani

Wasiliana na sisi

    Barabara ya Korogwe - Handeni

    Anuani ya Posta: S.L.P 51 HANDENI

    Simu ya Mezani: 027-2641807

    Simu ya Mkononi:

    Barua pepe: td@handenitc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera za faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Copyright ©2022 GWF . All rights reserved.