Katika jitihada za kuendelea na kupambana na uhaba wa vyumba vya madarasa katika Shule za Sekondari Halmashauri ya Mji handeni, "Msalagambo" umeendelea kushika kasi ambapo leo tarehe 05/10/2019 ilikuwa zamu ya Kata ya Mdoe ambapo Wananchi pamoja na Watumishi kutoka Ofisi ya Mkurugenzi pamoja na ya Mkuu wa Wilaya wamejitokeza kwa wingi kuchimba Msingi wa vyumba viwili (02) katika Shule ya Sekondari Handeni.
Diwani wa Kata ya Mdoe Mhe.Mwinshashi Ulenge akishiriki zoezi kuchimba Msingi Handeni Sekondari.
Mkurugenzi wa Halmashuri Bw.Kenneth Haule akishiriki kuchimba Msingi wa Vyumba vya Madarasa Handeni Sekondari
Wananchi waliojitokeza kwenye "Msalagambo" wakiendelea kuwajibika Shule ya Sekondari Handeni.
Pia Mbunge wa jimbo la handeni Mji mhe.Omari kigoda pamoja na Katibu Tawala wa Wilaya Bw.Boniphace Juma nao wameshiriki kwa ukamilifu kwenye "msalagambo" wa leo ili kuwatia hamasa wananchi kwenye jitihada za kuleta maendeleo hasa kwenye sekta ya Elimu, Halmashauri imejipanga kuhakikisha Wanafunzi wote waliofaulu mtihani wa Darasa la Saba wanajiunga na kidato cha kwanza.
Mbunge wa Handeni Mji mhe.Omari Kigoda akishiriki kuchimba msingi wa Ujenzi wa vyumba vya madarasa Handeni Sekondari
Katibu Tawala wa Wilaya ya Handeni Bw.Boniphace Juma akishiriki "msalagambo" katika Shule ya Sekondari Handeni
Barabara ya Korogwe - Handeni
Anuani ya Posta: S.L.P 51 HANDENI
Simu ya Mezani: 027-2641807
Simu ya Mkononi:
Barua pepe: td@handenitc.go.tz
Copyright ©2022 GWF . All rights reserved.