• Wasiliana na sisi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Handeni Town Council
Handeni Town Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Mji Handeni

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Fedha na Biashara
      • Mipango,Takwimu na Ufuatiliaji
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo,Umwagiliaji na Ushirika
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Elimu Msingi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Maji
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Ardhi na Maliasili
      • Elimu Sekondari
      • Usafi na Mazingira
    • Vitengo
      • Teknolojia,Habari na Mawasiliano
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • Ugavi
      • Nyuki
      • Sheria
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya kitalii
    • kilimo
    • ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • fedha na uongozi
      • mipango miji na mazingira
      • uchumi afya na elimu
      • ukimwi
      • maadili
    • Ratiba
      • vikao vya waheshimiwa madiwani
      • kuonana na mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma Kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Miongozo Mbalimbali
    • fomu mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za Shughuli za Ofisi au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha
    • Matukio

RAIS MAGUFULI KUMALIZA KERO YA MUDA MREFU YA UKOSEFU WA MAJI YA UHAKIKA KWA WAKAZI WA HANDENI MJINI

Posted on: August 7th, 2017

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe.Dkt John Pombe Magufuli ameahidi kumaliza kero ya upatikanaji wa Maji ya uhakika kwa Wananchi wa Handeni.

Ametoa ahadi hiyo leo alipokuwa akizungumza na Wananchi wa Handeni eneo la viwanja vya Kwambwembwele Handeni Mjini akitokea Tanga kwenye uwekaji wa jiwe la Msingi wa Bomba la mafuta linalounganisha Tanzania na Uganda.Amewaeleza Wananchi kuwa atahakikisha tatizo la Maji Handeni linatatuliwa kwa sababu kuna miradi mitatu ambayo inatarajiwa kuleta matokeo chanya ikiwemo mradi wa Bilioni 2.6 unaomalizikia utakaounganisha Maji maeneo ya Manga,Mkata na Handeni,mradi wa zaidi ya Bilion 200 Maji yatatolewa Mto pangani hivyo kumaliza tatizo la Maji.

Amewataka wakandarasi waliopo na wajao kufanya kazi kwa weledi na wakati ili kufikia malengo kwa wakati uliopangwa na kwamba  hatakuwa tayari kuwavumilia wakandarasi watakaokwamisha upatikanaji wa Maji ya uhakika Handeni."Wakandarasi mliopo na mtakaokuja mkitaka kugombana na mimi chezeni na miradi hii Maji Handeni" amesema Rais Dkt.John Magufuli.

Kwa upande mwingine amewataka Wananchi wa Handeni kuwa wavumilivu na kushirikiana vyema na watumishi wa kada ya Afya kwa sababu wanafanya kazi kubwa ya kuwahudumia Wagonjwa kulinganisha na idadi ndogo ya watumishi iliyopo,amewaeleza kuwa ajira zilisitishwa kwa muda kutokana na zoezi la uhakiki hivi punde watumishi wa Afya wataongezeka kwani kibali cha ajira kimekwishatolewa .Aidha amewataka Wananchi kujiunga na mfuko wa Bima ya Afya ili kuboresha huduma za Afya na kuhakikisha wanapata huduma kwa wakati pindi wanapohitaji kuhudumiwa.

Mwisho amepongeza Wananchi wa Handeni kwa namna wanavyojishughulisha na shughuli za kiuchumi hususani kilimo na ufugaji ambazo ni tija kwa maendeleo ya Taifa letu na kuwataka kuendelea na motisha ya kufanya kazi kwa juhudi huku wakiendelea kulinda na kuitunza Amani na Umoja wetu uliopo ili kuendeleza Taifa.Rais pia ameahidi kumalizia barabara inayounganisha Dumila na Handeni yenye urefu wa km 50 kwa kiwango cha lami ili kurahisisha shughuli za kiuchumi na usafirishaji.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt.John Pombe Magufuli amezungumza na Wananchi wa Handeni alipokuwa akimalizia ziara yake akitokea Tanga Mjini

Matangazo

  • KUITWA KWENYE USAILI 2 October 03, 2024
  • KUITWA KWENYE USAILI 1 September 27, 2024
  • TANGAZO LA MAJINA NA MIPAKA YA MITAA September 16, 2024
  • Angalia zaidi

Habari Mpya

  • HOSPITALI YA HALMASHAURI YA MJI HANDENI IMETOA ELIMU YA KUJINGA KWA MAGONJWA YA KUAMBUKIZA KWA WAFANYAKAZI WA BOMBA LA MAFUTA WILAYA YA HANDENI EACOP

    March 21, 2025
  • BARAZA MAALUMU LA MADIWANI LAPENDEKEZA KUONGEZEWA MAENEO YA UTAWALA

    March 14, 2025
  • MKUTANO MKUU WA 39 WA JUMUIYA YA TAWALA ZA MITAA TANZANIA (ALAT)

    March 11, 2025
  • ZIARA YA MHE. RAIS DKT SAMIA SULUHU HASSAN

    February 25, 2025
  • Angalia zaidi

Video

Mbunge wa jimbo la Handeni Mjini Mh.Reuben Kwagilwa aliamsha Bungeni
More Videos

Viunganishi vya Haraka

  • Dira na Dhamira
  • Kupata leseni ya Biashara
  • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
  • Kumuona Mkurugenzi
  • Kupata kibali cha Matangazo
  • Muundo wa Tasisi
  • Kumuona Mwenyekiti wa Halmashauri

Viunganishi Linganifu

  • Sekretariti ya Ajira
  • Ofisi ya Rais - Ikulu
  • FFARS-LIVE
  • PLANREP- BAJETI 2020/21
  • TAMISEMI
  • Utumishi

Watembeleaji wa Dunia

world map hits counter

Idadi ya waliotembelea tovuti

free HitCounter

Ramani

Wasiliana na sisi

    Barabara ya Korogwe - Handeni

    Anuani ya Posta: S.L.P 51 HANDENI

    Simu ya Mezani: 027-2641807

    Simu ya Mkononi:

    Barua pepe: td@handenitc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera za faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Copyright ©2022 GWF . All rights reserved.