• Wasiliana na sisi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Handeni Town Council
Handeni Town Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Mji Handeni

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Fedha na Biashara
      • Mipango,Takwimu na Ufuatiliaji
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo,Umwagiliaji na Ushirika
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Elimu Msingi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Maji
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Ardhi na Maliasili
      • Elimu Sekondari
      • Usafi na Mazingira
    • Vitengo
      • Teknolojia,Habari na Mawasiliano
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • Ugavi
      • Nyuki
      • Sheria
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya kitalii
    • kilimo
    • ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • fedha na uongozi
      • mipango miji na mazingira
      • uchumi afya na elimu
      • ukimwi
      • maadili
    • Ratiba
      • vikao vya waheshimiwa madiwani
      • kuonana na mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma Kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Miongozo Mbalimbali
    • fomu mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za Shughuli za Ofisi au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha
    • Matukio

UZINDUZI WA AWAMU YA PILI YA MRADI WA MAJI WA BWAWA LA KWAMAIZI:SERIKALI NA WADAU WALETA HUDUMA YA MAJI KARIBU NA WANANCHI

Posted on: January 21st, 2025

Mwenyekiti wa Halmashauri ya Mji Handeni, Mhe. Mussa Mkombati, ameongoza hafla ya uzinduzi wa awamu ya pili ya Mradi wa Bwawa la Kwamaizi. Hafla hii  ilihudhuriwa  na wadau mbalimbali wa maendeleo na wakazi wa Kata ya Kideleko.

Katika hotuba yake, Mhe. Mkombati ametoa shukrani kwa wadau wa maendeleo ambao Water Aid, OKF, HTM na Serengeti Breweries kwa kusaidia kufanikisha mradi huu wa usambazaji wa Maji kwa wananchi wa kata ya Kideleko.

Pia ametoa shukrani na pongezi kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, kwa kuweka mazingira wezeshi yanayowavutia wadau kushiriki katika miradi ya Maendeleo.

Mwenyekiti amesisitiza umuhimu wa ushiriki wa jamii katika kutekeleza mradi huu wa usambazaji maji na kuwataka wananchi kulinda vifaa vya mradi vitakavyofika ili kuhakikisha mradi unatekelezwa kwa wakati.

Pia amekumbusha umuhimu wa kujenga vyoo bora kama njia ya kulinda vyanzo vya maji, hasa katika kipindi cha mvua. Aidha  Mhe. Mkombati amesisitiza kuwa mafanikio ya awamu ya kwanza ya Mradi huu ni matokeo ya ushirikiano mkubwa wa wadau wote, lakini bado chanzo hiki cha maji kipo mbali na makazi ya wananchi, hivyo hitaji la miundombinu ya kuwafikishia maji karibu na makazi yao linabaki kuwa muhimu.

Katika awamu ya pili ya mradi, changamoto ya umbali wa chanzo cha maji na makazi ya wananchi itapunguzwa kwa kujenga miundombinu ya mabomba ya maji yenye urefu wa kilomita 3.5, tanki la kuhifadhia maji lita 100,000, chujio la kutibu maji, na vituo vitatu vya kuchotea maji vyenye mita za malipo. Pia, serikali itaongeza vituo zaidi vya maji kulingana na mahitaji ya jamii. Utekelezaji wa mradi huu pia utahusisha mafunzo na kampeni za usafi na uhifadhi wa mazingira kwa jamii, kuhakikisha matumizi endelevu ya maji na mazingira bora.

Mradi huu wa awamu ya pili umefadhiliwa na Operakallaren Foundation (OKF), iliyochangia shilingi milioni 359,633,851, huku serikali na wananchi wakitoa mchango wa vitendea kazi na nguvu kazi ili kufanikisha utekelezaji wa mradi kwa wakati.

Aidha, Katibu Tarafa wa Halmashauri ya Mji Handeni, Bi Julieth Mushi, alitoa shukrani kwa Water Aid na wadau wa maendeleo kwa kutekeleza mradi huu wa maji, akibainisha kuwa ni hatua kubwa inayosaidia kumtua mama ndoo kichwani na kuleta unafuu kwa wakazi wa eneo hilo.

Afisa Mazingira wa Halmashauri, Bwana Toba Mhina, alizungumzia umuhimu wa kupanda miti rafiki wa maji ili kulinda bwawa na kuimarisha uhifadhi wa maji, akieleza kuwa miti hiyo itasaidia pia katika kuzuia mmomonyoko wa ardhi.

Nae Diwani wa Kata ya Kideleko aliwashukuru Water Aid na OKF kwa kuleta mradi huu karibu na jamii na kuahidi ushirikiano kwa wadau wote waliofadhili mradi huu. Aliwahimiza wakazi kushiriki kikamilifu katika utekelezaji wa mradi na alisisitiza kuwa mradi huu utaleta faida ya muda mrefu kwa kizazi cha sasa na kijacho.

Matangazo

  • KUITWA KWENYE USAILI 2 October 03, 2024
  • KUITWA KWENYE USAILI 1 September 27, 2024
  • TANGAZO LA MAJINA NA MIPAKA YA MITAA September 16, 2024
  • Angalia zaidi

Habari Mpya

  • HOSPITALI YA HALMASHAURI YA MJI HANDENI IMETOA ELIMU YA KUJINGA KWA MAGONJWA YA KUAMBUKIZA KWA WAFANYAKAZI WA BOMBA LA MAFUTA WILAYA YA HANDENI EACOP

    March 21, 2025
  • BARAZA MAALUMU LA MADIWANI LAPENDEKEZA KUONGEZEWA MAENEO YA UTAWALA

    March 14, 2025
  • MKUTANO MKUU WA 39 WA JUMUIYA YA TAWALA ZA MITAA TANZANIA (ALAT)

    March 11, 2025
  • ZIARA YA MHE. RAIS DKT SAMIA SULUHU HASSAN

    February 25, 2025
  • Angalia zaidi

Video

Mbunge wa jimbo la Handeni Mjini Mh.Reuben Kwagilwa aliamsha Bungeni
More Videos

Viunganishi vya Haraka

  • Dira na Dhamira
  • Kupata leseni ya Biashara
  • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
  • Kumuona Mkurugenzi
  • Kupata kibali cha Matangazo
  • Muundo wa Tasisi
  • Kumuona Mwenyekiti wa Halmashauri

Viunganishi Linganifu

  • Sekretariti ya Ajira
  • Ofisi ya Rais - Ikulu
  • FFARS-LIVE
  • PLANREP- BAJETI 2020/21
  • TAMISEMI
  • Utumishi

Watembeleaji wa Dunia

world map hits counter

Idadi ya waliotembelea tovuti

free HitCounter

Ramani

Wasiliana na sisi

    Barabara ya Korogwe - Handeni

    Anuani ya Posta: S.L.P 51 HANDENI

    Simu ya Mezani: 027-2641807

    Simu ya Mkononi:

    Barua pepe: td@handenitc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera za faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Copyright ©2022 GWF . All rights reserved.