• Wasiliana na sisi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Handeni Town Council
Handeni Town Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Mji Handeni

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Fedha na Biashara
      • Mipango,Takwimu na Ufuatiliaji
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo,Umwagiliaji na Ushirika
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Elimu Msingi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Maji
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Ardhi na Maliasili
      • Elimu Sekondari
      • Usafi na Mazingira
    • Vitengo
      • Teknolojia,Habari na Mawasiliano
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • Ugavi
      • Nyuki
      • Sheria
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya kitalii
    • kilimo
    • ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • fedha na uongozi
      • mipango miji na mazingira
      • uchumi afya na elimu
      • ukimwi
      • maadili
    • Ratiba
      • vikao vya waheshimiwa madiwani
      • kuonana na mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma Kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Miongozo Mbalimbali
    • fomu mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za Shughuli za Ofisi au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha
    • Matukio

Walimu Halmashauri ya Mji Handeni, wapata mafunzo ya mfumo wa FFARS

Posted on: March 4th, 2023

Leo Jumamosi Tarehe 04/03/2023 Halmashauri ya Mji Handeni imehitimisha mafunzo ya siku mbili kuhusu mfumo wa kielektroniki wa malipo (FFARS) kwa walimu wa shule za msingi na sekondari. Katika mafunzo hayo mada mbalimbali zilifundishwa, ikiwemo namna ya kufanya uambatanishaji wa nakala za malipo, pamoja na namna ya kutumia mfumo huo. Mafunzo hayo yaliyofanyika katika ukumbi wa Halmashauri ya Mji Handeni yamehudhuriwa na walimu wakuu, wahasibu, mweka hazina na maafisa elimu msingi na sekondari.

Walimu wakisikiliza kwa umakini mada katika mafunzo ya mfumo wa FFARS yaliyofanyika Halmashauri ya Mji Handeni 

Katika semina hiyo Mhasibu wa Halmashauri ya Mji Handeni, ndugu John Sarus amewataka walimu wanaosimamia miradi na manunuzi ya vifaa mbalimbali vya shule, kuweka nyaraka zote muhimu pamoja na kuzitunza kwenye kabrasha husika na kupangilia katika taratibu maalum.

Nae Mkuu wa shule ya msingi Mapinduzi, ndugu Robert Njama amesema mafunzo ya FFARS na utunzaji wa nyaraka yamesaidia kufahamu mpangilio, utunzaji wa nyaraka za serikali na  hati mbalimbali za malipo, ameahidi kutokana na maelekezo yaliyotolewa na wataalam kutoka ofisi ya fedha, yeye kama msimamizi wa taasisi kuwa taratibu zote zitafuatwa ili kuepusha hoja ya taarifa juu ya malipo, wakati wa ukaguzi katika kipindi cha kila robo.

Mhasibu wa Halmashauri ya Mji Handeni, ndugu John Sarus akifafanua jambo,katika mafunzo ya mfumo wa FFARS uliofanyika Halmashauri ya Mji Handeni

Kwa wakati huohuo mkuu wa shule ya sekondari Kwenjugo, mwalimu Juma Abdurabi amesema kulikuwa na changamoto ya namna ya kupangilia nyaraka, kwenye kabrasha ambazo zilipelekea kuwa na hoja, wakati wa kupitia malipo ya kila robo. Na hatimaye kutokana na mafunzo haya yamesaidia kupata ufahamu, juu ya taratibu sahihi za kupangilia nyaraka hizo, pia ameishukuru Halmashauri ya Mji Handeni kwa kuendesha mafunzo hayo, ambapo yameweza kuwasaidia watumiaji wapya wa mfumo, kuufahamu na kujua namna ya kuutumia.

Kwa upande wake mwalimu wa fedha shule ya msingi Azimio Mwalimu.Agness Raphael amemshukuru Raisi wa Jamhuri ya muungano wa Tanzania, Dokta. Samia Suluhu Hassan kwa kuwawezesha walimu kwa kuwapatia vishikwambi, ambavyo vimekuja kutatua changamoto ya uhaba wa vifaa, hivyo wameweza kutumia mifumo mbalimbali kwa urahisi kutokana na vishikwambi hivyo.

Walimu wakiendelea kupatiwa mafunzo ya mfumo wa FFARS, katika ukumbi wa Halmashauri ya Mji Handeni

Hata hivo Mweka Hazina wa Halmashauri ya Mji Handeni, ndugu Mpakani Kassim amesema kuwa mafunzo yameenda vizuri na yameeleweka, mafunzo hayo yataongeza umakini kwenye utunzaji wa kumbukumbu za hati ya malipo. Na yamekuwa ni mafunzo yaliyowezeshwa kwa ajili ya kukumbusha, namna sahihi za kufanya malipo na manunuzi ya vifaa mbalimbali vya shule kupitia mfumo, ukizingatia kuwa  kuna maboresho yalifanyika juu ya mfumo huo siku za hivi karibuni, pia amewataka walimu waliohudhuria, kuzingatia mafunzo hayo ili kuhakikisha kuwa, wanayafanyia kazi mafunzo hayo na wanapata uzoefu.

Nae Mkurugenzi wa Halmashauri ya Mji Handeni Bi. Maryam Ukwaju amewaagiza walimu wa fedha wa shule zote, kuwa ndani ya wiki moja mpaka kufikia tarehe 10/03/2023 wawe wamekamilisha upangaji wa nyaraka zote za malipo za kuanzia mwezi Julai 2022 mpaka mwezi Februari 2023, kuzihakiki, kukamilisha bank reconciliation na kupitiwa pamoja na kuziwasilisha ili zipate kuhakikiwa na wahasibu wa Halmashauri


Abdulkadir Kassim

Handeni Mji

Matangazo

  • TANGAZO LA KAZI UJENZI WA JENGO LA DHARURA (EMD) HOSPITALI YA WILAYA HANDENI February 16, 2023
  • Angalia zaidi

Habari Mpya

  • Afisa elimu msingi: Kula shuleni ni lazima

    March 13, 2023
  • Maadhimisho ya siku ya wanawake duniani yafana, Halmashauri ya Mji Handeni

    March 08, 2023
  • Walimu Halmashauri ya Mji Handeni, wapata mafunzo ya mfumo wa FFARS

    March 04, 2023
  • MILIONI 63.6 ZAMWAGWA KWA WAJASIRIAMALI HANDENI MJI. RAIS SAMIA ATAJWA.

    March 03, 2023
  • Angalia zaidi

Video

Mbunge wa jimbo la Handeni Mjini Mh.Reuben Kwagilwa aliamsha Bungeni
More Videos

Viunganishi vya Haraka

  • Dira na Dhamira
  • Kupata leseni ya Biashara
  • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
  • Kumuona Mkurugenzi
  • Kupata kibali cha Matangazo
  • Muundo wa Tasisi
  • Kumuona Mwenyekiti wa Halmashauri

Viunganishi Linganifu

  • Sekretariti ya Ajira
  • Ofisi ya Rais - Ikulu
  • FFARS-LIVE
  • PLANREP- BAJETI 2020/21
  • TAMISEMI
  • Utumishi

Watembeleaji wa Dunia

world map hits counter

Idadi ya waliotembelea tovuti

free HitCounter

Ramani

Wasiliana na sisi

    Barabara ya Korogwe - Handeni

    Anuani ya Posta: S.L.P 51 HANDENI

    Simu ya Mezani: 027-2641807

    Simu ya Mkononi:

    Barua pepe: td@handenitc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera za faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Copyright ©2022 GWF . All rights reserved.