• Wasiliana na sisi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Handeni Town Council
Handeni Town Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Mji Handeni

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Fedha na Biashara
      • Mipango,Takwimu na Ufuatiliaji
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo,Umwagiliaji na Ushirika
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Elimu Msingi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Maji
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Ardhi na Maliasili
      • Elimu Sekondari
      • Usafi na Mazingira
    • Vitengo
      • Teknolojia,Habari na Mawasiliano
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • Ugavi
      • Nyuki
      • Sheria
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya kitalii
    • kilimo
    • ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • fedha na uongozi
      • mipango miji na mazingira
      • uchumi afya na elimu
      • ukimwi
      • maadili
    • Ratiba
      • vikao vya waheshimiwa madiwani
      • kuonana na mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma Kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Miongozo Mbalimbali
    • fomu mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za Shughuli za Ofisi au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha
    • Matukio

Wiki ya chanjo duniani, yazinduliwa Halmashauri ya Mji Handeni

Posted on: April 25th, 2023

Leo Jumanne tarehe 25/04/2023 Halmashauri ya Mji Handeni, imezindua rasmi wiki ya chanjo duniani ya mwaka 2023 yenye Kauli mbiu ”Tuwafikie wote kwa chanjo” na ujumbe ”jamii iliyopata chanjo, jamii yenye afya”. Hafla hiyo ya uzinduzi imefanyika katika kata ya Mabanda, kwenye Zahanati ya Misima. Ikihudhuriwa na viongozi mbalimbali wa Halmashauri ya Mji Handeni, watumishi wa Idara ya Afya na wananchi waliojitokeza kwa ajili ya kupata chanjo na elimu juu ya chanjo.

Mganga Mkuu wa Halmashauri ya Mji Handeni Dokta.Feisal Said, akiongea na wananchi waliohudhuria katika ghafla ya uzinduzi wa wiki ya chanjo duniani, uliofanyika katika kata ya Mabanda, Zahanati ya Misima

Akizungumza katika ghafla hiyo Mganga Mkuu wa Halmashauri ya Mji Handeni Dokta.Feisal Said, amewafahamisha wananchi juu ya umuhimu wa chanjo, ambao ni kujikinga dhidi ya magonjwa mbalimbali yanayoweza kupelekea vifo au ulemavu, hivyo kutokana na chanjo hizo na kuzingatia ukamilishaji wa dozi za chanjo wanaweza kuepukana na magonjwa hayo. Katika ghafla hiyo wazazi wenye watoto walio na umri chini ya miaka mitano wamesisitizwa kuwapeleka watoto hao kwa ajili ya kupata chanjo na kuwakumbusha wote ambao hawakupata chanjo ya UVIKO 19 kufika katika vituo husika kwa ajili ya kupata chanjo hiyo. Katika Halmashauri ya Mji Handeni, chanjo hizi zinatolewa katika vituo vya kutolea huduma za afya na shule ambazo zitatembelewa na kutolewa chanjo za kukinga saratani ya shingo ya kizazi kwa mabinti wa kuanzia umri wa miaka 14.

Mwenyekiti wa Halmashauri ya Mji Handeni Mhe.Mussa Mkombati, akiongea na wananchi waliohudhuria katika uzinduzi wa wiki ya chanjo duniani, uliofanyika katika kata ya Mabanda, Zahanati ya Misima

Kwa upande wake Mwenyekiti wa Halmashauri ya Mji Handeni Mhe.Mussa Mkombati, amefurahishwa na mahudhurio ya wazazi waloijitokeza kuwaleta watoto kwa ajili ya kupata chanjo ili kujikinga dhidi ya magonjwa mbalimbali, amempongeza Mganga Mkuu wa Halmashauri ya Mji Handeni Dokta.Feisal Said, kwa kufanya zoezi la chanjo kwa asilimia 112 katika mwaka 2022 na amewasisitiza kuendelea kutoa huduma bora kwa wananchi wa Halmashauri ya Mji Handeni, katika ghafla hiyo Mwenyekiti wa Halmashauri ya Mji Handeni aliendelea kusema kuwa kwa wale wote ambao hawajapata chanjo ya UVIKO 19, wajitokeze ili kuepukana na maradhi yanayopelekea kushindwa kupumua kwa urahisi na hatimaye kupelekea gharama kubwa ya matibabu yake. Akihitimisha Mhe.Mussa Mkombati, amewasisitiza wazazi juu ya kuwasimamia watoto katika malezi yenye maadili mema ili kuepukana na changamoto ya mmomonyoko wa maadili katika jamii.

Wananchi wa Halmashauri ya Mji Handeni waliohudhuria katika uzinduzi wa wiki ya chanjo duniani, uliofanyika katika kata ya Mabanda, Zahanati ya Misima

Nae Bi.Esther Laizer mkazi wa kata ya Mabanda, amemshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dokta.Samia Suluhu Hassan, kwa kuendelea kuwajali wananchi wake, kuwatatulia changamoto za vifaa na kuwasogezea huduma mbalimbali za jamii karibu na makazi yao, ikiwemo huduma ya afya ambapo kwa sasa wanaweza kupata huduma hizo bila kulazimika Kwenda umbali mrefu.

Abdulkadir Kassim

Handeni Mji

Matangazo

  • KUITWA KWENYE USAILI 2 October 03, 2024
  • KUITWA KWENYE USAILI 1 September 27, 2024
  • TANGAZO LA MAJINA NA MIPAKA YA MITAA September 16, 2024
  • Angalia zaidi

Habari Mpya

  • HOSPITALI YA HALMASHAURI YA MJI HANDENI IMETOA ELIMU YA KUJINGA KWA MAGONJWA YA KUAMBUKIZA KWA WAFANYAKAZI WA BOMBA LA MAFUTA WILAYA YA HANDENI EACOP

    March 21, 2025
  • BARAZA MAALUMU LA MADIWANI LAPENDEKEZA KUONGEZEWA MAENEO YA UTAWALA

    March 14, 2025
  • MKUTANO MKUU WA 39 WA JUMUIYA YA TAWALA ZA MITAA TANZANIA (ALAT)

    March 11, 2025
  • ZIARA YA MHE. RAIS DKT SAMIA SULUHU HASSAN

    February 25, 2025
  • Angalia zaidi

Video

Mbunge wa jimbo la Handeni Mjini Mh.Reuben Kwagilwa aliamsha Bungeni
More Videos

Viunganishi vya Haraka

  • Dira na Dhamira
  • Kupata leseni ya Biashara
  • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
  • Kumuona Mkurugenzi
  • Kupata kibali cha Matangazo
  • Muundo wa Tasisi
  • Kumuona Mwenyekiti wa Halmashauri

Viunganishi Linganifu

  • Sekretariti ya Ajira
  • Ofisi ya Rais - Ikulu
  • FFARS-LIVE
  • PLANREP- BAJETI 2020/21
  • TAMISEMI
  • Utumishi

Watembeleaji wa Dunia

world map hits counter

Idadi ya waliotembelea tovuti

free HitCounter

Ramani

Wasiliana na sisi

    Barabara ya Korogwe - Handeni

    Anuani ya Posta: S.L.P 51 HANDENI

    Simu ya Mezani: 027-2641807

    Simu ya Mkononi:

    Barua pepe: td@handenitc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera za faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Copyright ©2022 GWF . All rights reserved.