• Wasiliana na sisi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Handeni Town Council
Handeni Town Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Mji Handeni

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Fedha na Biashara
      • Mipango,Takwimu na Ufuatiliaji
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo,Umwagiliaji na Ushirika
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Elimu Msingi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Maji
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Ardhi na Maliasili
      • Elimu Sekondari
      • Usafi na Mazingira
    • Vitengo
      • Teknolojia,Habari na Mawasiliano
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • Ugavi
      • Nyuki
      • Sheria
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya kitalii
    • kilimo
    • ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • fedha na uongozi
      • mipango miji na mazingira
      • uchumi afya na elimu
      • ukimwi
      • maadili
    • Ratiba
      • vikao vya waheshimiwa madiwani
      • kuonana na mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma Kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Miongozo Mbalimbali
    • fomu mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za Shughuli za Ofisi au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha
    • Matukio

Mahindi ya bei nafuu yaanza kuuzwa Halmashauri ya Mji Handeni

Posted on: November 12th, 2022

Leo tarehe 12/11/2022 Halmashauri ya Mji Handeni imeanza rasmi kuuza mahindi ya bei nafuu kwa wakulima wa Halmashauri ya Mji Handeni katika ghala la ndugu Hafidhi linalopatikana maeneo ya njiapanda ya Kwabaya, kufuatia na uhaba na kuchelewa kwa msimu wa mvua kwa kipindi  kirefu iliyopelekewa na mabadiliko ya tabianchi na kusababisha upungufu wa chakula na kupanda kwa bei ya mazao ya chakula kwa wakulima, kufuatia hali hiyo serikali ya Jamhuri ya muungano wa Tanzania inahakikisha wananchi wanaendelea kupata chakula kwa kusambaza mahindi yanayopatikana kwa bei nafuu. Mahindi hayo yanauzwa kwa bei ya shilingi 898/= kwa kilogram moja ambapo kila kaya inaweza kununua mahindi hadi Kilogram zisizozidi 100.

Katika nyakati tofauti wananchi wa Halmashauri ya Handeni Mji wamemshukuru Rais wa Jamhuri ya muungano wa Tanzania Mh.Samia Suluhu Hassan kwa kuwapelekea chakula hicho katika maeneo yao kwa bei nafuu kulinganisha na bei ya wafanya biashara wa kawaida wanaouza chakula hicho kwa bei ya shilingi 1,300/= kwa kilogram  na kupelekea kushindwa kupata chakula cha kutosha kwa mahitaji ya wananchi  hususani kwa wananchi walio katika hali ngumu ya kiuchumi na wanufaika wa mfuko wa kusaidia kaya maskini TASAF.

Aidha Mtendaji Kata wa Kata ya Kideleko Bi.Asia Mussa Kasopa amemshukuru Mkuu wa Wilaya ya Handeni Bi.Siriel Mchembe kwa kuhakikisha kuwa mahindi hayo yanauzwa katika eneo ambalo ni rahisi kwa kila mwananchi kufika ili kuweza kununua mahindi hayo na kuhakikisha kuwa mahindi hayo yanauzwa kwa ajili ya chakula tu na si vinginevyo, Bi.Asia Kasopa amewashauri wananchi wote kuendelea kujitokeza kwa wingi kwa ajili ya kununua  mahindi kwani mahindi yapo kwa kiwango kikubwa na cha kutosha kwa kila mwananchi mwenye uhitaji wa chakula hicho.

Kwa upande wake Mhasibu msaidizi wa NRFA Dar-es-salaam Bi.Valeria Mwenda ameeleza kuwa zoezi la ununuzi limepokelewa kwa muitikio mkubwa sana na idadi ya kaya 44 zimefanikiwa kununua mahindi kwa siku ya kwanza ya zoezi hilo, kati ya kilogram 5 kwa kiwango cha chini mpaka kilogram 100 ambacho ni kiwango cha juu kabisa cha manunuzi ya mahindi kwa kaya moja na jumla ya tani 2.229 sawa na wastani wa kilogramu 50.659 kwa kaya, pia amewasisitiza watendaji kata/mitaa wawapatie utaratibu na kuwafahamisha bei elekezi ya kununua  mahindi hayo  ili kuepusha adha ya wakulima kufika eneo la manunuzi na kushindwa kufanya manunuzi kwa kukosa vigezo vya manunuzi ikiwemo kutokuwa na barua ya utambulisho na kuwalazimu kurudi kwenye uongozi husika na kupata barua za utambulisho, pia Bi.Valeria Mwenda amewakumbusha wananchi kuwa wanunuzi wote lazima wawasilishe barua zao za utambulisho kutoka kwenye uongozi wao wa kata/mitaa pindi wanapokuja kufanya manunuzi ili kuepusha udanganyifu na kuuza mahindi kwa matumizi ambayo sio ya chakula.

Mkurugenzi wa Halmashauri ya Mji Handeni Bi.Maryam Ukwaju anaendelea kuwakaribisha wananchi na wakazi wote wa Halmashauri ya Mji Handeni kwenye ununuzi wa mahindi ya bei nafuu unaoendelea katika ghala la ndugu Hafidhi linalopatikana maeneo ya njiapanda ya Kwabaya.

Abdulkadir Kassim

Handeni Mji.

Matangazo

  • KUITWA KWENYE USAILI 2 October 03, 2024
  • KUITWA KWENYE USAILI 1 September 27, 2024
  • TANGAZO LA MAJINA NA MIPAKA YA MITAA September 16, 2024
  • Angalia zaidi

Habari Mpya

  • HOSPITALI YA HALMASHAURI YA MJI HANDENI IMETOA ELIMU YA KUJINGA KWA MAGONJWA YA KUAMBUKIZA KWA WAFANYAKAZI WA BOMBA LA MAFUTA WILAYA YA HANDENI EACOP

    March 21, 2025
  • BARAZA MAALUMU LA MADIWANI LAPENDEKEZA KUONGEZEWA MAENEO YA UTAWALA

    March 14, 2025
  • MKUTANO MKUU WA 39 WA JUMUIYA YA TAWALA ZA MITAA TANZANIA (ALAT)

    March 11, 2025
  • ZIARA YA MHE. RAIS DKT SAMIA SULUHU HASSAN

    February 25, 2025
  • Angalia zaidi

Video

Mbunge wa jimbo la Handeni Mjini Mh.Reuben Kwagilwa aliamsha Bungeni
More Videos

Viunganishi vya Haraka

  • Dira na Dhamira
  • Kupata leseni ya Biashara
  • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
  • Kumuona Mkurugenzi
  • Kupata kibali cha Matangazo
  • Muundo wa Tasisi
  • Kumuona Mwenyekiti wa Halmashauri

Viunganishi Linganifu

  • Sekretariti ya Ajira
  • Ofisi ya Rais - Ikulu
  • FFARS-LIVE
  • PLANREP- BAJETI 2020/21
  • TAMISEMI
  • Utumishi

Watembeleaji wa Dunia

world map hits counter

Idadi ya waliotembelea tovuti

free HitCounter

Ramani

Wasiliana na sisi

    Barabara ya Korogwe - Handeni

    Anuani ya Posta: S.L.P 51 HANDENI

    Simu ya Mezani: 027-2641807

    Simu ya Mkononi:

    Barua pepe: td@handenitc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera za faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Copyright ©2022 GWF . All rights reserved.