• Wasiliana na sisi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Handeni Town Council
Handeni Town Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Mji Handeni

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Fedha na Biashara
      • Mipango,Takwimu na Ufuatiliaji
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo,Umwagiliaji na Ushirika
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Elimu Msingi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Maji
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Ardhi na Maliasili
      • Elimu Sekondari
      • Usafi na Mazingira
    • Vitengo
      • Teknolojia,Habari na Mawasiliano
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • Ugavi
      • Nyuki
      • Sheria
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya kitalii
    • kilimo
    • ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • fedha na uongozi
      • mipango miji na mazingira
      • uchumi afya na elimu
      • ukimwi
      • maadili
    • Ratiba
      • vikao vya waheshimiwa madiwani
      • kuonana na mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma Kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Miongozo Mbalimbali
    • fomu mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za Shughuli za Ofisi au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha
    • Matukio

UJENZI BWAWA LA KWAMAIZI WAFIKIA 90% SERENGETI BREWERIES YATOA MILIONI 380

Posted on: May 2nd, 2023

Mradi wa ujenzi wa bwawa la Kwamaizi uliopo mtaa wa Kwamaizi, kata ya Kideleleko, Halmashauri ya Mji Handeni ulioanza kujengwa mwezi februari mwaka huu ambao unatarajia kugharimu kiasi cha shilingi milioni 380 utakapokamilika, fedha zilizotolewa na kampuni ya bia ya Serengeti Breweries Limited, umefikia asilimia 90 ya ujenzi wake na unatarajia kukamilika mwishoni mwa mwezi huu wa tano.

Akizungumza katika hafla ya utoaji vyeti kwa wahitimu wanawake 24 wanaounda Kikundi Cha Maendeleo cha Kata ya Kideleko, Meneja Mawasiliano na Uendelevu wa SBL, Bi.Rispa Hatibu amesema bwawa hilo litakapokamilika linatarajiwa kuwa na ukubwa wa mita za ujazo 135 na kuhifadhi maji ya kuwatosheleza zaidi ya wakazi 2000 wa eneo la mtaa wa Kwamaizi pamoja na maeneo ya jirani.

“Tunao washirika wetu katika huu mradi ambao ni WaterAID, wao wanasimamia usalama wa huu mradi lakini niwaombe wananchi wa Kwamaizi na wote watakaonufaika na huu mradi, tunzeni chanzo hiki cha maji”alisisitiza

Mkuu wa Miradi kutoka WaterAID Dkt. Happiness Wilbroad amesema shirika lao kwa zaidi ya miaka 40 limekuwa likitekeleza miradi ya kufikisha huduma ya maji safi na salama kwa jamii, na katika kuhakikisha miradi hiyo inakuwa endelevu jamii hushirikishwa katika utekelezaji wa miradi, na katika ujenzi wa bwawa la Kwamaizi, kikundi cha wanawake 24 wa Kwamaizi wamepewa mafunzo ya utunzaji mazingira kulizunguka bwawa pamoja na mafunzo ya ujasiriamali ikiwemo utengenezaji wa sabuni za maji.

Mkuu wa wilaya ya Handeni Wakili Albert G. Msando ametoa shukrani kwa uongozi wa kampuni ya bia ya Serengeti, kwa ufadhili wa mradi huo lakini pia kwa usimamizi na kuhakikisha mradi unakamilika kwa wakati. Halikadhalika, amewapongeza shirika la WaterAID kwa usimamizi wao wa karibu na uratibu tangu mradi unaanza hadi sasa.

Pia, aliishukuru ofisi ya Mkurugenzi wa Halmashauri ya Mji Handeni kwa ushirikiano wa karibu inaoutoa, akitolea mfano mafunzo ya kikundi cha wanawake 24 kuratibiwa na Ofisi ya Mkurugenzi kupitia Idara ya Maendeleo ya jamii. Kuhusu kikundi cha wanawake, amewataka wakawe mabalozi wazuri juu ya utunzaji wa mazingira katika bwawa mara baada ya kupatiwa mafunzo hayo ambayo leo hii wamehitimu na kukabidhiwa vyeti

Matangazo

  • KUITWA KWENYE USAILI 2 October 03, 2024
  • KUITWA KWENYE USAILI 1 September 27, 2024
  • TANGAZO LA MAJINA NA MIPAKA YA MITAA September 16, 2024
  • Angalia zaidi

Habari Mpya

  • HOSPITALI YA HALMASHAURI YA MJI HANDENI IMETOA ELIMU YA KUJINGA KWA MAGONJWA YA KUAMBUKIZA KWA WAFANYAKAZI WA BOMBA LA MAFUTA WILAYA YA HANDENI EACOP

    March 21, 2025
  • BARAZA MAALUMU LA MADIWANI LAPENDEKEZA KUONGEZEWA MAENEO YA UTAWALA

    March 14, 2025
  • MKUTANO MKUU WA 39 WA JUMUIYA YA TAWALA ZA MITAA TANZANIA (ALAT)

    March 11, 2025
  • ZIARA YA MHE. RAIS DKT SAMIA SULUHU HASSAN

    February 25, 2025
  • Angalia zaidi

Video

Mbunge wa jimbo la Handeni Mjini Mh.Reuben Kwagilwa aliamsha Bungeni
More Videos

Viunganishi vya Haraka

  • Dira na Dhamira
  • Kupata leseni ya Biashara
  • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
  • Kumuona Mkurugenzi
  • Kupata kibali cha Matangazo
  • Muundo wa Tasisi
  • Kumuona Mwenyekiti wa Halmashauri

Viunganishi Linganifu

  • Sekretariti ya Ajira
  • Ofisi ya Rais - Ikulu
  • FFARS-LIVE
  • PLANREP- BAJETI 2020/21
  • TAMISEMI
  • Utumishi

Watembeleaji wa Dunia

world map hits counter

Idadi ya waliotembelea tovuti

free HitCounter

Ramani

Wasiliana na sisi

    Barabara ya Korogwe - Handeni

    Anuani ya Posta: S.L.P 51 HANDENI

    Simu ya Mezani: 027-2641807

    Simu ya Mkononi:

    Barua pepe: td@handenitc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera za faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Copyright ©2022 GWF . All rights reserved.