• Wasiliana na sisi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Handeni Town Council
Handeni Town Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Mji Handeni

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Fedha na Biashara
      • Mipango,Takwimu na Ufuatiliaji
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo,Umwagiliaji na Ushirika
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Elimu Msingi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Maji
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Ardhi na Maliasili
      • Elimu Sekondari
      • Usafi na Mazingira
    • Vitengo
      • Teknolojia,Habari na Mawasiliano
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • Ugavi
      • Nyuki
      • Sheria
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya kitalii
    • kilimo
    • ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • fedha na uongozi
      • mipango miji na mazingira
      • uchumi afya na elimu
      • ukimwi
      • maadili
    • Ratiba
      • vikao vya waheshimiwa madiwani
      • kuonana na mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma Kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Miongozo Mbalimbali
    • fomu mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za Shughuli za Ofisi au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha
    • Matukio

Ifahamu programu ya Shule Bora

Posted on: December 12th, 2022

Kwa watoto wote

Mradi wa Shule Bora umelenga kuiunga mkono Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania katika kuinua kiwango cha elimu jumuishi pamoja na kuweka mazingira salama ya kujifunzia kwa wanafunzi wote wa kike na wa kiume katika shule za Serikali za Tanzania.

Kwa ushirikiano na Serikali ya Tanzania mradi huu utafanya maboresho yatakayowezesha kila mtoto kupata msingi mzuri katika elimu yake ya awali, ili kuitumia fursa kwa kutoa mchango wake katika ukuaji wa nchi na maendeleo yake.

Changamoto zitakaposhughulikia

Wakati watoto wengi wakijiunga na kuendelea na masomo, matokeo ya elimu Tanzania yamekuwa na changamoto nyingi. Ni asilimia nane tu (8%) ya wanafunzi katika elimu ya msingi wanafikia kiwango cha Taifa cha kujua kusoma kwa ufasaha, 12% wanafikia kiwango cha Taifa cha kuwa na ujuzi wa kujumlisha na kutoa.

Kwa kiasi fulani hii inachangiwa na ongezeko la uhitaji wa elimu msingi sambamba na ongezeko la idadi ya watu kunakopelekea ongezeko la uwiano wa walimu na wanafunzi, ambako kwa sasa ni wastani wa wanafunzi sitini na mbili kwa kila mwalimu mmoja kwa shule za msingi za Serikali.

Afisa Elimu Mkoa wa Tanga Mwl.Ewapo Mkisi akizungumza na waandishi wa habari siku ya mafunzo juu ya programu ya shule bora katika ukumbi wa Korogwe Executive, Tanga.


Unalenga matokeo

Katika ngazi ya kitaifa Shule Bora itatoa msaada wa kiufundi kwa Serikali ya Tanzania, pamoja na utekelezaji wa mradi wa wafadhili wa lipwa kwa matokeo yaani Education Program for Result II (EPforRII).

Malengo ya utekelezaji wa kitaifa kuwa yanapangwa kwa pamoja kati ya Serikali na wafadhili huku utoaji wa fedha ukihusisha malengo yaliyofikiwa. Hii inasisimua mabadiliko ya kimfumo kama yale ya msawazo sawa wa walimu na ugawaji wa vitabu.

Shule Bora pia itafadhili matokeo muhimu yatakayotokana na vigezo vilivyothibitishwa toka katika mradi wa EPforR ambavyo vitatumika katika utoaji wa fedha na wafadhili wengine.

Kwa ufadhili wa Serikali ya Uingereza kupitia mfuko wa UK aid, gharama za mradi zitakuwa na bajeti ya paundi za kiingereza 89 millioni, sawa na shilingi za kitanzania bilioni 271 na utafanya kazi katika ngazi zote za mradi. Mradi huu wa Shule Bora utatekelezwa hadi ifikapo mwaka 2027.

Ushirikiano na ubunifu

Shule bora itafanya kazi moja kwa moja na mamlaka za Serikali za Mikoa na Halmashauri pamoja na shule katika Mikoa tisa yenye changamoto nyingi kama ilivyopendekezwa na kukubalika na Serikali ya Tanzania; katika kuboresha elimu. Inakadiriwa kuwa mradi huu utawafikia watoto takribani Milioni Nne wa kitanzania, kati yao nusu ni wasichana.

Mabadiliko ya ubunifu yataonekana na kutathminiwa katika ngazi za chini ambazo walengwa muhimu watapatikana katika shule zote za msingi Tanzania.


Shule bora inalenga katika mambo manne;

1
Kujifunza
Watoto wote wanajifunza katika shule.
2
Kufundisha
Mfuko wa msaada wa UK utaunga mkono na kuimarisha kazi ya ufundishaji Tanzania.
3
Jumuishi
Kuhakikisha kuwa watoto wote wa kitanzania mashuleni wanakuwa katika mazingira salama na rafiki ili kuwawezesha kumaliza elimu ya msingi na  wanaendelea na elimu ya Sekondari;na
4
Kujenga mfumo
Mfuko wa UK Aids utaunga mkono Serikali na kuimarisha ili kupata au kuwa na thamani ya fedha katika utoaji wa elimu katika ngazi zote toka chini hadi Tifani.


Mikoa ambayo Programu ya shule bora inatekelezwa

Jumuishi ni kipaumbele cha Shule Bora

Mradi utawatupia macho kwa karibu wanafunzi wa kike, wanafunzi wenye mahitaji maalum na wale wanaotoka katika mazingira magumu. Mradi pia utashughulikia mambo yatakayowezesha watoto kuwa shuleni katika mazingira bora na salama ili kuwapa nafasi ya kujifunza na kuendelea na masomo yao ya Sekondari.

Hii ni pamoja na kuwashirikisha wazazi na jumuiya katika kuboresha usalama wa shule na kuondoa migogoro,kuhakikisha kuwa walimu wanazungumzia mambo ya jinsia na upatikanaji wa mahitaji ya wanafunzi wenye uhitaji maalumu.

Pia kutayarisha mazingira salama na kuwaunga mkono wasichana kushiriki pamoja na kujadili mambo yanayowahusu pamoja na kuwasaidia katika kipindi cha hedhi.

Mradi wa Shule Bora utaisaidia Tanzania kutengeneza mfumo wa elimu utakaofanana na wa UK ambao utawezesha kuondoka(kuziba) pengo kati ya wasichana na wavulana kwa kiasi kikubwa na kwa maeneo mengi wasichana kwa sasa wanalingana na wavulana katika kujiunga elimu ya msingi,viwango vya kusoma na kuandika pia.

Na uzuri zaidi idadi ya wasichana wanaohitimu elimu ya msingi na sekondari inaizidi ile ya wavulana.

Mipango ya mfuko wa UK aids pia imeimarisha ubora wa elimu na mafunzo kwa watoto wapatao milioni 3.1

Tathmini iliyofanywa ilionekana kuwa juhudi za mfuko wa UK aids zilichangia ongezeko la watoto takribani mara mbili Zaidi kuliko wale ambao walikuwa nje ya jitihada za mfuko huo.

Mpango kazi wa kwanza wa utekelezaji wa mradi wa Shule Bora baada ya uzinduzi utajumuisha jitihada zitakazopelekea;

  • Kuunga mkono walimu katika matumizi ya mbinu za ufundishaji katika mfumo wa ‘pedagojies”.
  • Kuunga mkono Serikali katika kuwabainisha na kutathimini watoto wenye mahitaji maalumu.
  • Kutoa usaidizi kwa Serikali kwenye mipango yake ya kielimu na mahitaji ya vituo vinavyotoa usaidizi kwa watoto wenye ualbino na uoni hafifu
  • Kutoa vifaa saidizi vya kufundishia 3R’s kwa watoto wenye tatizo la kuona na kusikia.
  • Kutoa mafunzo kwa watoto wenye tatizo la mtindio wa ubongo na (autism)


Mradi wa Shule Bora ni zao la mfuko wa UKAID kwa Serikali ya Tanzania ikilenga kuunga mkono miradi ya elimu Tanzania. Unatekelezwa katika Mikoa tisa ya Tanzania kwa kupokea utaalamu wa kiufundi toka Cambridge Education ikishirikiana na mashirika ya ADD International, International Rescue Committee na Plan International.

Kwa taarifa Zaidi; www.camb-ed.com au barua pepe:CETanzania@camb-ed.com, na simu: +255 759957880


Handeni Mji

Matangazo

  • KUITWA KWENYE USAILI 2 October 03, 2024
  • KUITWA KWENYE USAILI 1 September 27, 2024
  • TANGAZO LA MAJINA NA MIPAKA YA MITAA September 16, 2024
  • Angalia zaidi

Habari Mpya

  • HOSPITALI YA HALMASHAURI YA MJI HANDENI IMETOA ELIMU YA KUJINGA KWA MAGONJWA YA KUAMBUKIZA KWA WAFANYAKAZI WA BOMBA LA MAFUTA WILAYA YA HANDENI EACOP

    March 21, 2025
  • BARAZA MAALUMU LA MADIWANI LAPENDEKEZA KUONGEZEWA MAENEO YA UTAWALA

    March 14, 2025
  • MKUTANO MKUU WA 39 WA JUMUIYA YA TAWALA ZA MITAA TANZANIA (ALAT)

    March 11, 2025
  • ZIARA YA MHE. RAIS DKT SAMIA SULUHU HASSAN

    February 25, 2025
  • Angalia zaidi

Video

Mbunge wa jimbo la Handeni Mjini Mh.Reuben Kwagilwa aliamsha Bungeni
More Videos

Viunganishi vya Haraka

  • Dira na Dhamira
  • Kupata leseni ya Biashara
  • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
  • Kumuona Mkurugenzi
  • Kupata kibali cha Matangazo
  • Muundo wa Tasisi
  • Kumuona Mwenyekiti wa Halmashauri

Viunganishi Linganifu

  • Sekretariti ya Ajira
  • Ofisi ya Rais - Ikulu
  • FFARS-LIVE
  • PLANREP- BAJETI 2020/21
  • TAMISEMI
  • Utumishi

Watembeleaji wa Dunia

world map hits counter

Idadi ya waliotembelea tovuti

free HitCounter

Ramani

Wasiliana na sisi

    Barabara ya Korogwe - Handeni

    Anuani ya Posta: S.L.P 51 HANDENI

    Simu ya Mezani: 027-2641807

    Simu ya Mkononi:

    Barua pepe: td@handenitc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera za faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Copyright ©2022 GWF . All rights reserved.