• Wasiliana na sisi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Handeni Town Council
Handeni Town Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Mji Handeni

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Fedha na Biashara
      • Mipango,Takwimu na Ufuatiliaji
      • Mifugo na Uvuvi
      • Kilimo,Umwagiliaji na Ushirika
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Elimu Msingi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Maji
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Ardhi na Maliasili
      • Elimu Sekondari
      • Usafi na Mazingira
    • Vitengo
      • Teknolojia,Habari na Mawasiliano
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • Ugavi
      • Nyuki
      • Sheria
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya kitalii
    • kilimo
    • ufugaji
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu za Halmashauri
      • fedha na uongozi
      • mipango miji na mazingira
      • uchumi afya na elimu
      • ukimwi
      • maadili
    • Ratiba
      • vikao vya waheshimiwa madiwani
      • kuonana na mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma Kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Miongozo Mbalimbali
    • fomu mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za Shughuli za Ofisi au Kitaifa
    • Hotuba za Viongozi Mbalimbali
    • Maktaba ya Picha
    • Matukio

Ziara ya Mwenyekti wa Halmashauri ya Mji Handeni kwenye nyumba za ibada yaendelea

Posted on: May 14th, 2023

Katika kikao cha madiwani cha tarehe 28/4/2023, moja ya Agenda waliyokubaliana ni kupita kwenye nyumba za ibada na kuhamasisha na kuelezea namna ambayo maadili yamepotea kwenye jamii yetu. Katika kufanikisha hili leo tarehe 14/05/2023 Mwenyekiti wa Halmashauri ya Mji Handeni Mhe Musa Mkombati (Diwani), aliendelea na ziara yake kwenye makanisa ya Kideleko, Kwaluwala, Kwamgome, Majeshi majeshi na E.A.G.T -Kwamngumi. Kwenye ziara hiyo Mhe Diwani aliongozana na Bi Amina Waziri (Afisa Maendeleo ya Jamii) kwa niaba ya Mkurugenzi wa Halmashauri ya Mji Handeni.

Mhe. Mwenyekiti wa Halmashauri ya Mji Handeni amewataka viongozi wa dini kushirikiana na wazazi, walezi pamoja na walimu kuwaongoza katika kupambana na janga hili, vilevile aliwaeleza kuwa “mmomonyoko wa maadili hasa vitendo vya ushoga, ndoa za utotoni pamoja na mapenzi ya jinsia moja vinafadhiliwa na watu wenye nguvu za kifedha, hivyo basi mtu mmoja mmoja hawezi kupambana nao ndio maana tumeamua kutumia viongozi wa dini katika vita hii”. Wakati huohuo amewashauri wazazi kuwa makini na ndugu wa karibu wanapokuja kutembelea nyumbani, maana matendo mengi ya ubakaji yanatokea kwa watu wa karibu, hivyo basi aliwataka wageni wasiachwe kulala na watoto kwenye chumba kimoja.

Pia amewaambia watoto wakatae na watoe taarifa kwa walimu, wazazi na viongozi wa dini pindi wanapofanyiwa matendo ya unyanyasaji.

Alimalizia kwa kusema Handeni bila Ndoa za Utotoni, ushoga na ndoa za jinsia moja inawezekana

 

Mwenyekiti wa Halmasahuri Mhe.Musa Mkombati  (Diwani) akizungumza na waumini katika Kanisa la Majeshi Majeshi juu ya mmomonyoko wa maadili katika jamii yetu.

 

Nae Afisa Maendeleo ya Jamii Bi. Amina Waziri, aliwaasa waumini  kulea watoto kwenye misingi ya mtoto wa mwezako ni wako, na sio kama ilivyo sasa kusema ”Asiyefunzwa na mamae atafunzwa na ulimwengu” tuachane na maneno au dhana hiyo, kwa nguvu za pamoja tunaweza kuondoa janga hili.

Pia aliwaasa wazazi kuzungumza na watoto wao mara kwa mara kujua matatizo yao na sio kujishughulisha na kazi pamoja na kutafuta pesa

Bi Amina Waziri (Afisa Maendeleo ya Jamii) akitoa neno la utangulizi kabla ya kumkaribisha Mwenyeketi wa Halmashauri kuja kuongea na waumini wa Kanisa la Kideleko kushoto ni mwenyeji wake diwani wa kata ya Kideleko Mhe.Godfrey Munga

Pia Padre William Mkeni wa Kanisa la Kideleko, ameshukuru jitihada zinazofanywa na serikali na kuahidi kuunga mkono juhudi hizo, zenye tija katika kuimarisha maadili mema katika jamii. Alihitimisha kwa kuwakumbusha waumini kwa kusema “Mungu alisema nendeni mkajaze ulimwengu sio kwa ndoa za jinsia moja bali ni kwa mke na mume”.

Padre William Mkeni wa Kanisa la Kideleko akitoa neno la shukurai kwa mgeni rasmi 

Matangazo

  • KUITWA KWENYE USAILI 2 October 03, 2024
  • KUITWA KWENYE USAILI 1 September 27, 2024
  • TANGAZO LA MAJINA NA MIPAKA YA MITAA September 16, 2024
  • Angalia zaidi

Habari Mpya

  • HOSPITALI YA HALMASHAURI YA MJI HANDENI IMETOA ELIMU YA KUJINGA KWA MAGONJWA YA KUAMBUKIZA KWA WAFANYAKAZI WA BOMBA LA MAFUTA WILAYA YA HANDENI EACOP

    March 21, 2025
  • BARAZA MAALUMU LA MADIWANI LAPENDEKEZA KUONGEZEWA MAENEO YA UTAWALA

    March 14, 2025
  • MKUTANO MKUU WA 39 WA JUMUIYA YA TAWALA ZA MITAA TANZANIA (ALAT)

    March 11, 2025
  • ZIARA YA MHE. RAIS DKT SAMIA SULUHU HASSAN

    February 25, 2025
  • Angalia zaidi

Video

Mbunge wa jimbo la Handeni Mjini Mh.Reuben Kwagilwa aliamsha Bungeni
More Videos

Viunganishi vya Haraka

  • Dira na Dhamira
  • Kupata leseni ya Biashara
  • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
  • Kumuona Mkurugenzi
  • Kupata kibali cha Matangazo
  • Muundo wa Tasisi
  • Kumuona Mwenyekiti wa Halmashauri

Viunganishi Linganifu

  • Sekretariti ya Ajira
  • Ofisi ya Rais - Ikulu
  • FFARS-LIVE
  • PLANREP- BAJETI 2020/21
  • TAMISEMI
  • Utumishi

Watembeleaji wa Dunia

world map hits counter

Idadi ya waliotembelea tovuti

free HitCounter

Ramani

Wasiliana na sisi

    Barabara ya Korogwe - Handeni

    Anuani ya Posta: S.L.P 51 HANDENI

    Simu ya Mezani: 027-2641807

    Simu ya Mkononi:

    Barua pepe: td@handenitc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera za faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Copyright ©2022 GWF . All rights reserved.